Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Janga la dawa za kulevya lajadiliwa UN

Janga la dawa za kulevya lajadiliwa UN

Viongozi wa serikali na wanaharakati wanaohudhuria mkutano wa kujadili tatizo la dawa za kulevya duniani wamehimizwa kupiga marufuku hukumu ya kifo na kuimarisha huduma za matibabu kwa watumiaji wa dawa za kulevya.
Katika mkutano wa kwanza wa kimataifa kujadili suala la dawa za kulevya kuwahi kuandaliwa katika kipindi cha miongo miwili iliyopita, baraza kuu la Umoja wa Mataifa hapo jana lilipitisha rasimu inayobadili mfumo unaotumika wa kupambana na dawa za kulevya ulioanzishwa miaka ya sabini ambapo hatua kali za kutumia nguvu za kisheria na kulifanya tatizo la dawa za kulevya kuwa uhalifu.

Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO Margaret Chan amesema sera kuhusu matumizi ya dawa ambazo zinatuama zaidi katika matumizi ya mfumo wa kulikabili janga hilo kama uhalifu unahitaji kupanuliwa na kujumuisha sasa mtazamo wa afya ya umma.

Mkutano huo maalum uliitishwa na Colombia, Mexico na Guatemala ambazo zinakumbwa na athari za matumizi na biashara ya dawa za kulevya ambazo zimechochea uhalifu mkubwa na ghasia katika nchi hizo.

Sera zilizopo zimefeli
Rais wa Mexico, Enrique Pena Nieto amesema vita dhidi ya dawa za kulevya sharti vitizamwe kwa jicho la kuzingatia haki za binadamu na kuonya kuwa adhabu kali kwa watumiaji wa dawa hizo unasababisha mkondo usiokoma wa watu kuhisi kutengwa na kusababisha uhalifu.

Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto

Nieto anaunga mkono kutoharamishwa kwa matumizi ya bangi inapotumika kama tiba na kwa masuala ya tafiti za kisayansi. Pakistan imesema inatiwa wasiwasi mkubwa na hatua ya kutaka kuhalalisha matumizi ya bangi na dawa nyingine za kulevya.

Uruguay ndiyo ilikuwa nchi ya kwanza kuhalalisha kikamilifu matumizi ya bangi mnamo mwaka 2013 na Canada ni miongoni mwa nchi zinazopanga pia kuhalalisha matumizi yake
.
Wajumbe kutoka Umoja wa Ulaya, Uswisi, Brazil, Costa Rica na Uruguay wametaka kuondolewa kwa adhabu ya kifo kwa wanaopatikana na hatia ya kuhusika katika biashara ya dawa za kulevya, adhabu inayotumika sana China, Iran na Indonesia.

Kulingana na WHO, takriban watu milioni 27 duniani wanaishi na athari za kiafya za matumizi ya dawa za kulevya na wengine laki nne wanakufa kila mwaka kutokana na matumizi ya dawa hizo.

Kujidunga dawa za kulevya kwa kutumia sindano kunachangia kwa asilimia 30 ya maambukizi mapya ya virusi vya HIV na inachangia pia katika maambukizi ya Hepatatis B na C duniani.

Matumaini yapo kwa waraibu wa dawa za kulevya
Chan amesema kuna matumaini kwa wanaotumia dawa hizo kwani wanaweza kusaidiwa kupata matibabu na ushauri nasaha na kurejeshwa katika jamii kuchangia katika kuleta maendeleo.

Dawa ya kulevya ya Cocaine Dawa ya kulevya ya Cocaine

Wiki iliyopita, mawaziri wa zamani wa Mexico, Colombia na Nigeria walijumuika na watu mashuhuri Sting na Mochael Dougals pamoja na mwekezaji Warren Buffet kutoa wito wa kukomeshwa kwa kampeni ambayo imeleta athari zaidi kuliko manufaa katika vita dhidi ya dawa za kulevya.

Barua waliyoiandika kwa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon imesema mtazamo mpya wa dunia kuhusu namna ya kushughulikia tatizo la dawa za kulevya unazingatia kuwa na huruma, haki za binadamu, sayansi na afya unahitajika.

Licha ya makubaliano mapana ya haja ya kuwa na mtazamo mpya, kuna migawanyiko mikubwa miongoni mwa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu ni njia ipi bora ya kulikabili janga hilo.

Nchi kadhaa za Amerika ya Kusini zinasema hatua za kutumia adhabu na sheria kali imeshindwa, na imesababisha vifo na kuwaharibu maelfu ya watu duniani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.