Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Jeshi la Polisi nchini limetajwa kuwa kinara wa ukiukaji wa haki za Binadamu kwa raia,

Jeshi la Polisi nchini limetajwa kuwa kinara wa ukiukaji wa haki za Binadamu kwa raia, ikidaiwa kukithiri kwa vitendo  vya kutesa raia pindi.

Hayo yamesemwa leo na Kamishina wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora Dk. Kevin Mandopi wakati  wa kuadhimisha siku ya  Afrika ya kuzinduliwa kwa muongozo wa Luanda kuhusu haki za watuhumiwa wa makosa ya Jinai, wanaokamatwa na kuzuiliwa mahabusu kabla ya kushtakiwa.

DKT KELVIN MANDOPI

Amesema kwa mujibu wa taarifa mbali mbali za tume hiyo, pamoja na malalamiko yanayo pokelewa na tume kutoka kwa wananchi dhidi ya Jeshi la Polisi ni zaidi ya asilimia 60 ya malalamiko yanayo pelekwa Jeshi la Polisi kwa kukiuka haki za binadamu.

Amefafanua kuwa licha ya sheria ya Jeshi la Polisi ya mwaka 2002 kifungu cha 27(3) kuwapa mamlaka polisi kumkamata mtu yeyote  iwapo kunasababu za kisheria kufanya hivyo lakini amedai jeshi limetumia sheria hiyo kufanya uvunjifu wa haki za Binadamu.  POLISI HAKI ZA BINADAMU

Dk Mandopi ametaja uvunjifu huo wa haki za badamu unaofanywa na jeshi la Polisi ni pamoja na kupigwa kwa Raia pindi wanapokamatwa,kutofikishwa Mahakamani kwa kubabikiziwa kesi,kunyimwa dhamana kutofikishwa mahakamani kwa wakati kupigwa,kuteswa pamoja na kucheleweshwa kwa upelelezi.

Dk Mandopi amesema mambo hayo  ni kinyume na matakwa ya muongozo wa Luanda, katiba, sheria za nchi mikataba ya kikanda na kimataifa ya haki za bindamu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.