Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Maadhimisho ya siku ya uhuru bila ya furaha Afrika Kusini


Maoni: Maadhimisho ya siku ya uhuru bila ya furaha Afrika Kusini

Katika maadhimisho ya siku ya uhuru nchini Afrika Kusini chama cha ANC hakikuonyesha furaha. Katika maoni yake mkuu wa idara ya Afrika Claus Stäcker anasema hali hiyo inatokana na kashfa za Rais Jacob Zuma
Malalamiko dhidi ya Rais Jacob Zuma bungeni Malalamiko dhidi ya Rais Jacob Zuma bungeni

Viongozi wa chama cha ANC bado wanajaribu kufanya mbinu za kuikabili hali iliyotokea .Bado wanajaribu kuzidhibiti athari za madhara yaliyosababishwa na Rais Zuma. Na bado wanaamini kuwa wataweza kupata suluhisho la ndani ili na hivyo kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa mnamo mwezi wa Agosti kwa mafaniko.

Lakini hakuna mwenye mashaka tena ndani ya chama cha ANC kwamba Zuma amekuwa mzigo usiobebeka. Ndani kwa ndani mapambano yanaendelea miongoni mwa wajanja, ya kugombania vyeo na viti vyao bungeni vinavyowahakikishia mishahara mizuri. Zuma amefanikiwa kujenga mtandao wa kifisadi ambao mpaka sasa umeweza kumlinda ili asianguke.

Chama cha Mandela kinajimaliza chenyewe
Watu wa nje wamepigwa na butaa kuona jinsi chama cha ANC, cha akina Luthuli,Tambo na Mandela kilivyoendelea kufarakana na malengo yake ya hapo awali. Watu wanashangaa kuona jinsi chama hicho kinavyojimaliza chenyewe haraka. Vyama vyingine vya ukombozi vilichukua muda wa miaka 50 kufikia hatua hiyo.

Baadhi ya wanachama waadilifu bado wanasisitiza juu ya moyo wa mshikamano wa hapo awali. Wanajaribu kuufufua kutokea ndani ya chama.Na kwenye mikutano ya faragha wanazungumza kinagaubaga! Wanalalamika juu ya utovu wa heshima na majikwezo ya viongozi wao walioivuruga imani yote ya chama cha ANC.
Mkuu wa idara ya Afrika Claus Stäcker Mkuu wa idara ya Afrika Claus Stäcker

Watu hao wanasema ni kosa kuwaita watu wanaomkosoa Zuma kuwa wasaliti na wanalalamika kwamba viongozi wao wanayatelekeza maadili yanayokipa chama nguvu. Makada wa chama wanaomtupa mkono Zuma wazi wazi wanaongezeka waliopambana na utawala wa makaburu, waliofungwa jela pamoja na Mandela na mawaziri wa sasa.

Na sasa kashfa ya Nkandla
Zuma alitumia mamilioni ya fedha za umma kukikarabati kijiji chake binafsi katika jimbo la Kwa -Zulu. Hukumu iliyotolewa na mahakama dhidi ya Zuma lilikuwa pigo kubwa. Zuma ameariwa kurudisha Euro Milioni 14.

Katika nchi nyingine Zuma angelilazimika kujiuzulu kwa hiari yake. Na hata sasa hiyo ingelikuwa njia bora kabisa ya kukiwezesha chama cha ANC kusonga mbele kama jumuiya ya umma. Hata hivyo njia bora zaidi ingelikuwa kumtimua Zuma.

Chama cha ANC kilikuwa na uwezo, wa kujibadilisha lakini sasa chama hicho tawala kimeipoteza nguvu hiyo. Kamati Kuu ya ANC imegawanyika juu ya suala la Zuma, lakini kwa bahati mbaya katika misingi ya ukabila .Tofauti kama hizo hazikuwapo hapo awali. Njia nyingine ni kusonga mbele kama hapo awali.Kutokana na kuwa na wabunge wengi, Zuma ana ngao thabiti bungeni, licha ya kukiuka katiba.

Pengo kati ya chama cha ANC na jamii nzima linazidi kupanuka na hivyo chama hicho kinazidi kutetereka kutoka kwenye misingi ya demokrasia.

Nkosazana Dlamini-Zuma
Njia nyingine inayowezekana ni kwa Zuma kung'atuka kimyakimya na kumwachia urithi Nkosazana Dlamini - Zuma aliewahi kuwa mkewe, anaemaliza muhula wake wa uenyekiti wa Umoja wa Afrika mnamo mwezi Julai. Mama huyo anayo sifa ya kuwa mchapa kazi na pia anakubalika katika pande zote za ANC. Tofauti na mwanasiasa mwengine, Cyril Ramaphosa anaeungwa mkono na matajiri.
Nkosazana Dlamini- Zuma atakabiliwa na jukumu la kuirejesha imani ya chama. Hizo zinaweza kuwa habari nzuri katika siku ya leo inayoadhimishwa kuwa ya uhuru nchini Afrika kusini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.