Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MALEMA ATUHUMIWA KWA UHAINI

ANC yamtuhumu Malema kwa uhaini
Chama tawala nchini Afrika Kusini ANC kimemtuhumu kiongozi wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF),Julius Malema kwa uhaini.
Kiongozi huyo wa EFF anadaiwa kusema ''kuwa serikali ya rais Jacob Zuma inapaswa kukoma kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wanaoandamana kwa amani la sivyo itang'olewa madarakani kwa mtutu wa bunduki.
''Matamshi hayo ni ya kutishia amani na utangamano nchini Afrika Kusini kwa hakika hayo ni matamshi ya uhaini na hatua kali zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya Malema'' msemaji wa ANC Zizi Kodwa alisema.

''Tunaiomba serikali ichukue hatua kali zaidi dhidi ya matamshi hayo ilikuzuia visa vya utovu wa usalama''
Katika mahojiano ya moja kwa moja na shirika la habari la Al Jazeera, bw Malema, alisema kuwa matokeo ya uchaguzi wa 2014 katika jimbo la Gauteng hayakuwa ya haki na akaonya dhidi ya wizi wa kura katika uchaguzi ujao wa kimkoa.
Uchaguzi huo wa mashinani unatarajiwa kufanyika mwezi Agosti.

''Sehemu moja ya wajibu wetu wa mapinduzi ni kupigana na iwapo itatubidi ,hatutakuwa na ila bali kuchukua silaha na kutetea haki zetu.Tutapigana. alisema bw Malema.

Chama tawala cha ANC kinamtuhumu Malema kwa kukiuka kanuni za kitaifa za uchaguzi kwa kuwachochea watu wapigane.

Kodwa alisema kuwa hiyo ni kinyume cha sheria ya nchi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.