Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Suarez ampiku Ronaldo kwa mabao



Suarez
Atletico na Real Madrid zimezidi kuiongezea presha Barcelona, lakini mabingwa hao wa La Liga wamezidi kukaza buti mbio za ubingwa msimu huu Suarez akitenda miujiza

Barcelona imeendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa La Liga baada ya kuiadhibu Sporting Gijon kwa kichapo cha 6-0 Real Madrid na Atletico nazo zikiendelea kushinda mechi zao za wikiendi.
Kutoka kwenye majanga ya vipigo, Barcelona imekuja na moto mkali kwa ushindi mkubwa kwenye mechi mbili mfululizo wakianza na ule wa bao 8-0 dhidi ya Diportivo kabla ya ushindi wa Jumamosi usiku.

Messi alianza kuzifungua kamba za Sporting Gijon mapema kipindi cha kwanza akifunga bao moja pekee kati ya mabao sita yaliyofungwa kwenye mchezo huo.

Baadaye Luis Suarez alipachika bao la pili na matokeo kuwa 2-0. Penalti mbili za haraka-haraka zilizofungwa na Suarez ziliyafanya matokeo kuwa 4-0.

Dakika tano kabla ya mchezo kumalizika ikapatikana penalti nyingine ambayo iliwekwa kimiani na Neymar hivyo kuifanya safu ya ushambuliaji ya Barca (MSN) kila mmoja kufunga bao kwenye mchezo huo


Suarez akapiga bao lake la nne kwenye mchezo huo dakika za lala salama na kukamilisha ushindi wa Barcelona 6-0 Sporting Gijon.

Kwa mwendo huo hadi sasa, Luis Suarez amefikisha mabao 34 Cristiano Ronaldo akiendelea kubaki na mabao yake 31 baada ya kukosa mechi ya Rayo Vallecano. Mbio za tuzo ya Pichichi! 


Zikiwa zimesalia mechi tatu, Barcelona inaongoza ligi kwa pointi 82 sawa na Atletico Madrid huku Real Madrid ikifuatia kwa pointi zake 81.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.