Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Trump na Clinton watafuta kura katika majimbo matano

 
Wamarekani katika majimbo matano ya kaskazini mashariki watapiga kura hii leo katika uchaguzi wa mchujo wa kuteua wagombea urais wa vyama vya Republican na Democratic. 
Mgombea Urais wa chama cha Democrats Hillary Clinton ataazimia katika chaguzi hizo za leo kupanua pengo kati yake na Bernie Sanders huku mgombea urais kwa upande wa Republican Donald Trump akiwa na uhakika wa kuendelea kuongoza katika kinyang'anyiro cha kupata tiketi ya chama chake licha ya wapinzani wake kuungana dhidi yake.

Chaguzi hizo za mchujo zinafanyika katika majimbo ya Connecticut, Delaware, Maryland, Pennsylvania na Rhode Island. Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani Bi Clinton anatumai kuibuka na ushindi katika majimbo hayo na hivyo kuendeleza ndoto yake yake ya kuwa Rais wa kwanza mwanamke nchini Marekani.

Clinton ana imani atashinda
Akihutubu katika jukwaa la manispaa ya Philadelphia jana usiku, Clinton amesema bado hawajapata uteuzi na hivyo watatia bidii sana kuwashawishi wapiga kura hadi vituo vitakapofungwa.

  Mgombea Urais wa Democrats Bernie Sanders

Trump pia alikuwa akifanya kampeni kabambe katika majimbo hayo matano muhimu kujaribu kufikisha idadi ya wajumbe 1,237 wanaohitajika kumuwezesha kupata tiketi ya kupeperusha bendera ya chama cha Republican katika uchaguzi wa Rais unaotarajiwa mwezi Novemba mwaka huu.

Wapinzani wake Ted Cruz na John Kasich wameungana kujaribu kutatiza ndoto ya Trump ya kugombea urais.

Kulingana na mapatano kati ya wagombea hao wawili, Kasich hatafanya kampeni katika jimbo la Indiana ambalo linafanya uchaguzi wa mchujo tarahe 3 mwezi ujao na kwa upande wake Cruz hatatafuta kura katika majimbo la New Mexico na Oregon ili kuzigawanya kura ambazo angepata Trump.

Trump amewakosoa wapinzani wake kwa kula njama ya kumbwaga akisema mapatano yao yanaonyesha ni kwa kiasi gani wako dhaifu na wanatapatapa.

Cruz na Kasich waungana kumbwaga Trump
Kulingana na taifiti za kura ya maoni ziliofanywa na shirika la habari la CBS, Trump anaongoza kwa asilimia 40 kwa umaarufu miongoni mwa wapiga kura Indiana, huku Cruz akiungwa mkono kwa asilimia 35 na Kasich asilimia 20.

Wagombea urais wa Republican Trump, Cruz na Kasich  
Wagombea urais wa Republican Trump, Cruz na Kasich

Cruz na Kasich wamekiri kuwa matumaini yao ya kuibuka washindi ni kuungana katika kumzuia Trump kupata wajumbe 1, 237 kabla ya mkutano mkuu wa chama.

Cruz hata ameanza kutafuta mgombea mwenza. Mwenyekiti wa kampeini zake Chad Sweet amesema Cruz ameanza kuwatathimini wagombea kadhaa watakaochukua wadhifa wa makamu wa Rais akiwemo mfanyabiashara Carly Fiorina.

Trump anapigiwa upatu kushinda katika majimbo yote matano yanayoshiriki katika chaguzi za mchujo leo naye Sanders ambaye kampeni zake mashinani zimeshika kasi, anabashiriwa atajitahidi vilivyo kumtoa kijasho Clinton hasa katika jimbo la Connecticut

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.