Gunners wameishiwa mbinu na Kocha wao Mfaransa
amezidi kuchanganyikiwa huku akiwa na hofu ya kushindwa kufuzu michuano
ya Ligi ya Mabingwa Uefa
Arsenal walishindwa kuwafunga Paka Weusi, ambao pointi moja katika uwanja wao wa nyumbani imewapa tumaini la kupona kushuka daraja.
Petr Chech alilazimika kuokoa shuti kali kutoka kwa Wahbi Khazri na Jermain Defoe, Arsenal wakishindwa kuonyesha umahiri wa kikosi chao kutumia nafasi walizopata.
Matokeo hayo yanaifanya Arsenal kubakia nafasi ya nne, pointi tano mbele ya Manchester United – ambao wana mchezo mmoja mkononi hali inayomfanya Wenger kuwa na hofu katika mechi zilizo mbele yao, moja ikiwa ni dhidi ya Manchester City na nyingine dhidi ya Norwich inayohaha kujiokoa kushuka daraja.
Alipoulizwa kama anahofu Arsenal itapoteza fursa ya kupata nafasi ya 4-bora, Wenger alisema: “Naam, ndiyo. Tunaogopa kwa sababu haya ni mapambano.
“Kuna ligi mbili kwa sasa: timu tunazodhani ni rahisi – unakuta zinacheza vizuri, zikiwa zinapambana kuepuka kushuka daraja, na mchezo unakuwa tofauti.
“Inaumiza kwa sababu tunacheza ili kushinda taji na hali halisi kwamba hatushindi ni moja ya mambo yanayoleta kero, sawa natimu nyingine nyingi
.
“Timu kama Sunderland wapo tayari kupambana kufa na kupona, na hawakati tamaa dakika zote 90.
“Walianza kwa hofu na tungeweza kutumia udhaifu huo walioanza nao, lakini hatukuweza ukizingatia tulicheza Jumapili, Alhamisi, na leo [Jumapili], tulikuwa na uchovu kiasi fulani na matokeo yakawa hivyo.”

Maoni
Chapisha Maoni