Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA 2-1 MGAMBO LIVE KUTOKA UWANJA WA TAIFA (FULL TIME)

Mwamuzi anamaliza mchezo, Yanga 2, Mgambo 1

Dakika ya 90+2

Dakika ya 90+1: Yanga wanashambuliwa.

Dakika ya 90. Zimeongezwa dakika mbili za nyongeza.

Dakika ya 89: Mchezo unaendelea.

Dakika ya 86: Yanga wanapata kona, Kaseke anapiga lakini kipa anaokoa.

Dakika ya 84: Mgambo wanamiliki mpira kwa dakika moja sasa.

Dakika ya 82: Yanga wanaongoza mabao 2-1, Tambwe ameshindwa kutumia nafasi ya wazi ya kufunga bao.

Dakika ya 79: Mgambo wanafanya mabadiliko, anatoka Nassor Gumbo anaingia Ally Nassor.
 

Dakika ya 73: Yanga wanafanya mabadiliko, anatoka Niyonzima anaingia Thaban Kamusoko.

Kaseke anaipatia Yanga bao la pili baada ya kutokea piga nikupige katika lango la Mgambo, mpira ukamkuta Kaseke akiwa mwenyewe, akapiga shuti kali na kuwa bao la pili kwa Yanga na kwake pia katika mchezo wa leo.

Dakika ya 71: Kasekeeeeeee
 
Dakika ya 63: Kamusoko ambaye leo yuko benchi anapasha misuli.

Dakika ya 60: Mgambo wanapata faulo nje ya eneo la 18, wanapiga lakini inashindwa kuwa na faida.

Dakika ya 55: Mgambo wanafanya mashambulizi ya nguvu lakini wanashindwa kutumia nafasi.

Dakika ya 50: Ngoma tena anakosa bao la wazi baada ya kupewa pasi na Tambwe, tayari Ngoma alishaanza kushangilia akijua mpira unaingia wavuni.

Dakika ya 47: Ngoma anashindwa kumalizia mpira uliokuwa ukipita mbele kidogo ya lango la Mgambo.

Dakika ya 45: Yanga wanafanya mabadiliko ametoka Paul Nonga, ameingia Donald Ngoma.

Kipindi cha pili kimeanza

Mpira ni mapumziko

Dakika ya 45: Yanga wanafanya shambulizi la nguvu lakini Simon Msuva anashindwa kumalizia mpira.

Dakika ya 44: Kiungo Deusi Kaseke anaisawazishia Yanga kwa kuumalizia mpira uliopigwa kwa kichwa na Amiss Tambwe kutoka upande wa kulia, mabeki wa Mgambo wanabaki wanatazamana.

Kasekeeeeeeeee

Dakika ya 37: Mchezo unaendelea
 
Dakika ya 35: Mchezo umesimama, kipa wa Mgambo kaumia.

Dakika ya 34: Mvua imekatika, timu zote zinashambuliana kwa zamu, mpira umemilikiwa zaidi na viungo wa timu zote.
 

Dakika ya 30: Msuva anakatwa ndani ya eneo la hatari la Mgambo lakini mwamuzi anapeta.

Dakika ya 27: Salum Telela anapewa kadi ya njano kutokana na kucheza faulo.

Dakika ya 26: Mgambo wanaendelea kuwa wagumu kukubali ngome yao kupitika.

Dakika ya 23: Mchezo unaendelea.

Juma Abdul ilionyesha kuwa na maumivu na alitoka akiwa anachechemea.

Dakika ya 21: Yanga wanafanya mabadiliko, anatoka Juma Abdul anaingia Mbuyu Twite.

Dakika ya 21: Kipa wa Mgambo, Said Hamis ameumia na yupo chini, mchezo umesimama.

Dakika ya 19: Mgambo wanafanya shambulizi lakini inakuwa offside.

Dakika ya 15: Mgambo wanazuia vizuri lango lao kutokana na Yanga kuonekana kutafuta bao kwa nguvu.

Dakika ya 10: Yanga wameamka na kuanza kushambulia lango la Mgambo. 

Bao hilo limefungwa dakika ya 4, mfungaji ni Bolly Ajaly

Dida alimuanzishia mpira Telela ambaye alishindwa kuumiliki na kujikuta akinyang'anywa na washambuliaji wa Mgambo ambao walitumia nafasi hiyo kutupia mpira wavuni

Mgambo wanapata bao kutokana na uzembe wa kiungo wa Yanga, Salum Telela.


Dakika ya 3: Timu zote zinacheza mchezo wa kusomana, mchezo bado haujachangamka.


Mchezo umeanza


Timu ndiyo zinaingia uwanjani kwa ajili ya kuanza mchezo.


Idadi ya watu siyo wengi sana uwanjani kutokana na mvua kunyesha jijini Dar es Salaam, mpaka sasa kuna manyunyu eneo hili la Uwanja wa Taifa.


KIKOSI CHA YANGA:
Deogratius Munish ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Salum Telela, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Paul Nonga, Amissi Tambwe, Deus Kaseke.

WANAOANZIA BENCHI
Benedict Tinocco, Mbuyu Twite, Vincent Bossou, Matheo Anthony, Donald Ngoma, Thaban Kamusoko, Mwinyi Hajji.

 
KIKOSI CHA MGAMBO:
Said Hamis, Salum Mlima, Chande Magonja, Henry Chacha, Bakari Mtama, Salum Kipanga, Nassor Gumbo, Mohammed Samatta, Herbert Lukindo, Bolly Ajaly, Salum Gila.

WANAOANZIA BENCHI
Mudathir Hamis, Bushiru Mohammed, Francis, Anyosisye, Ally Nassoro, Nurdin Mkomeni, Uda Bakari, Abuu Daud.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.