Kiungo
mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Ajib Migomba anatarajia kuanza majaribio
katika klabu ya Golden Arrows ya Afrika Kusini, kesho.
Tayari Ajib yuko jijini Durban ambako ni makao makuu ya klabu hiyo iliyoanzishwa mwaka 1943.
Meneja wa Ajib, Juma Ndambile amesema mchezaji wake huyo atafanya majaribio katika kikosi cha Arrows kuanzia kesho.
“Kesho
ndiyo siku anaanza majaribio, leo Arrows wana mechi. Kesho ndiyo
ataungana nao na baada ya hapo tutaangalia nafasi nyingine,” alisema.
“Wakala
wake amempa nafasi ya kufanya majaribio katika klabu nyingine ya daraja
la kwanza ya Amazulu. Hii itakuwa ni baada ya Arrows kutoa majibu yao
au wanaonaje,” alisema.
Ajib
aliondoka nchini bila ruhusa ya uongozi wa Simba, inaelezwa Ndambile
ndiye alimpigia simu Rais wa Simba, Evans Aveva kwamba mchezaji huyo
anaondoka siku inayofuata.
Siku
hiyo jioni, Ajib alikuwa amelambwa kadi nyekundu ya kujitakia wakati
Simba ilipofungwa na Mwadui FC ya Shinyanga kwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam.
11
May
2016


Maoni
Chapisha Maoni