Mrithi wa Stewart Hall ameshapatikana Azam FC, ni makocha wawili kutoka Hispania, Zeben Hernandez na Jonas Garcia
Mtendaji mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba amesema, wameamua kufanya hivyo baada ya kufikia makubaliano na makocha hao wa Hispania na kutaka kuziba pengo la Hall, ambaye tayari wameshamruhusu kuondoka.
“Tumekamilisha zoezi la kocha mpya na tayari tumewasainisha mikataba ya miaka miwili makocha wetu Zeben Hernandez atakayekuwa kocha mkuu wakati na Jonas Garcia yeye atakuwa kocha wa viungo huku Denis Kitambi akiendelea kuwepo kama kocha msaidizi na ndiye atakuwa mwenyeji wao nchini wakati watakapoanza majukumu yao mapya,”amesema Kawemba.
Baada ya kukamilisha dili lao makocha hao watarejea Hispania baada ya kushuhudia mchezo wa mwisho wa ligi kati ya Azam FC dhidi ya Mgambo JKT pamoja na ule wa FA Cup dhidi ya Yanga, baada ya hapo watarejea nchini kwa ajili ya kuanza majukumu yao kama makocha wapya wa Azam.
Maoni
Chapisha Maoni