Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Boko Haram bado ni kitisho cha usalama


Hollande: Boko Haram bado ni kitisho cha usalama

Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema Boko Haram bado ni kitisho licha ya hatua za kuridhisha za kijeshi zilizochukuliwa kuliangamiza kundi hilo la waasi lenya ngome yake nchini Nigeria.
Akizungumza katika mkutano wa kilele kujadili kitisho hicho cha Boko Haram mjini Abuja, Nigeria, Hollande amesema matokeo ya operesheni dhidi ya Boko Haram ni ya kuridhisha kwani waasi hao wamekatwa makali na kulazimika kurudi nyuma.

Nigeria ni mwenyeji wa mkutano huo wa kilele wa kujaidli kitisho kinachosababishwa na uasi huo wa Boko Haram, mkutano unaowaleta pamoja viongozi wa Ufaransa, Cameroon, Niger, Benin na Niger.

Na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Philiph Hammond, naibu wa waziri wa mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken, maafisa wa jumuiya za Afrika magharibi na kati na maafisa wa Umoja wa Ulaya.

Miaka saba ya uasi kaskazini mashariki mwa Nigeria, imesababisha mauaji ya watu takriban 20,000 na kuwaacha wengine milioni 2.6 bila ya makaazi na kusababisha mzozo wa kibinadamu

Boko Haram ikabiliwe vipi?
Mazungumzo katika mkutano wa kilele wa usalama unatarajiwa kuangazia kutumwa rasmi kwa kikosi cha wanajeshi wa nchi za kanda hiyo ya magahraibi mwa Afrika kinachohusisha Nigeria na majirani zake kukabiliana na Boko Haram.
Rais wa Cameroon Paul Biya na Rais wa Nigeria Muhamadu Buhari Rais wa Cameroon Paul Biya na Rais wa Nigeria Muhamadu Buhari

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea wasiwasi wake kuhusu mafungamano kati ya kundi hilo la Boko Haram na kundi la wanamgambo wenye itikadi kali wa Dola la Kiislamu IS baada ya ripoti kuwa kuna wapiganaji wa kutoka Nigeria wanaopigana vita vya kijihadi Libya.
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa mafungamano hayo ni kitisho kwa usalama barani Afrika.

Baraza la usalama hapo jana Ijumaa limesema mazungumzo ya Abuja yanapaswa kuunda mkakati madhubuti wa kushughulikia uongozi, usalama, maendeleo na usaidizi wa kiuchumi, kijamii na kibinadamu kuushughulikia mzozo uliosababishwa na uasi wa Boko Haram katika kanda hiyo.

Kiongozi wa Boko Haram Abubakar Shekau mwaka jana alitangaza kuwa mtiifu kwa kiongozi wa IS Abu Bakr Al Baghdad. Ufaransa imetoa mafunzo na vifaa kama sehemu ya juhidi za kimataifa za kuisaidia Nigeria kukabiliana na Boko Haram. Hollande na Buhari wametia saini makubaliano ya kuimarisha ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili.

Hammond pia ameonya kuwepo kitisho kikubwa kutokana na mafungamano ya Boko Haram na IS lakini amesema kuna ufanisi katika kukabiliana na makundi hayo kufuatia usaidizi kutoka kwa Ufaransa, Uingereza na Marekani.

Waziri huyo wa mambo ya nje wa Uingereza amesema huu sio wakati wa kulegeza kamba katika vita dhidi ya Boko Haram na kuna haja ya kurejesha uthabiti katika kanda hiyo ya magharibi mwa Afrika.

Mkutano huo wa kilele, unakuja miaka miwili baada ya mwingine wa ngazi ya juu kufanyika Paris. Jeshi la Nigeria limekuwa likipambana vikali na waasi wa Boko Haram katika siku za hivi karibuni katika msitu wa Sambisa ambao ni ngome ya waasi hao.

Je Buhari atawaangamiza waasi?
Rais Buhari ameapa kulishinda kundi hilo kabla ya kumaliza mwaka mmoja tangu aingie madarakani. Jeshi la Nigeria limetangaza kundi hilo linasambaratika. Hata hivyo naibu wa waziri wa mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken amesema haionekani kama Boko Haram limeshindwa.
Kiongozi wa Boko Haram Abubakar Shekau Kiongozi wa Boko Haram Abubakar Shekau

Kutumwa kwa kikosi cha wanajeshi 8,500 wa kikanda kitakachojumuisha wanajeshi kutoka Nigeria, Benin, Cameroon, Chad na Niger kunatarajiwa kuwepo miongoni mwa ajenda kuu za mkutano huo.

Kikosi kinachoungwa mkono na Umoja wa Afrika kilicho na makao yake katika mji mkuu wa Chad, N'djamena kilipaswa kuanza kufanya operesheni dhidi ya Boko Haram mwezi Julai mwaka jana.

Boko Haram imetanua mashambulizi yake nje ya Nigeria, na mara kadha imezishambulia, Cameroon, Niger na Chad. Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Samantha Power amesema watu milioni 9.2 katika nchi hizo wameathirika na mzozo huo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.