Ruka hadi kwenye maudhui makuu

De Gea: Tunataka Kushinda Kombe la FA

De Gea: Tunataka Kushinda Kombe la FA

David De Gea ametamka kuwa 2015-16 ulikuwa msimu mzuri kwake Manchester United lakini anataka kumaliza na taji
Mlinda mlango wa Manchester United David De Gea amesema amekuwa na msimu mzuri katika taaluma yake ya soka kwa mtazamo wake, lakini anataka kumaliza japo na taji moja katika mechi ya fainali Kombe la FA Jumamosi.

De Gea alikaribia kuondoka Old Trafford siku ya mwisho kabla ya kufungwa dirisha la usajili wa majira ya joto kutimkia Real Madrid lakini mkanganyiko wa nyaraka ukamkwamisha.
Lakini hakutaka mambo ya usajili yamvuruge, aliendelea kufanya kazi yake nzuri United, na amechangia kwa kiwango kikibwa kuiwezesha Manchester United kutinga fainali ya Kombe la FA na kumaliza nafasi ya tano Ligi Kuu.

Ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa United kwa mara ya tatu, na kuwa kipa wa pili Ligi Kuu Uingereza huku wa kwanza akiwa Czech wa Arsenal.
“Umekuwa msimu bora katika maisha yangu ya soka,” alisema De Gea. “Niko vizuri kimwili na kiakili.

“Kama tukitwaa Kombe la FA utakuwa msimu mzuri. Sote tunataka kutwaa taji hilo muhimu kwa ajili ya mashabiki wetu na kwa ajili yetu binafsi kama wachezaji. Tutapambana hadi mwisho na kufanya kila kinachowezekana kutwaa taji hilo.”

Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amesema kutwaa Kombe la FA kutaisaidia United kumaliza msimu mgumu waliokuwa nao kwa furaha na huenda ukajenga bahati kwa ajili ya msimu ujao.
“Tumekuwa na msimu mgumu na tumedhamiria kuibuka na kombe,” aliongeza.
“Na kushinda kutatupa kila sababu ya kujivuna na kutuongezea hamasa na tumaini la kufanya makuu zaidi.”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.