Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Interview ya kwanza ya Mourinho kama kocha wa Man U

Interview ya kwanza ya Mourinho kama kocha wa Man U

Jose-first interview at utd
Jose Mourinho amewaasa mashabiki wa Manchester United kusahau yote yaliyotokea miaka mitatu iliyopita wakati timu hiyo ilipokuwa chini ya David Moyes na Louis van Gaal na kuangalia namna ya kuirudisha upya katika zama zake.

Mourinho amethibitishwa leo na Man United rasmi kuwa kocha klabu hiyo akichukua mikoba ya Mholanzi Louis Van Gaal baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu.

Mourinho anakabiliwa na mtihani mzito wa kuirudisha United katika zama za ubora wake chini ya Sir Alex Ferguson na kurudisha tena imani kwa mashabiki.

“Tunaweza kuingalia timu yetu katika sehemu mbili,” alisema Mourinho, “sehemu ya kwanza ni miaka mitatu iliyopita na nyingine ni historia inayobeba klabu hii.

“Nadhani ningependa kusahau kilichotokea ndani ya miaka mitatu iliyopita, napenda kuangalia timu kubwa (Man United) ambayo ipo mikononi mwangu kwa sasa na nadhani mashabiki wanachosubiri kusikia kutoka kwangu ni kusema kuwa nataka ushindi. Nadhani wachezaji wanahitaji kusikia nikisema- hivi, Nataka kushinda”.

“Najisikia vizuri. Nadhani hiki ni kipindi sahihi kuipokea klabu hii kwa sababu ni moja ya vilabu ambayo unahitaji kujiandaa ili kuweza kufanya vyema, ndiyo maana naiita klabu kubwa.

“Na klabu kubwa lazima ipate kocha mkubwa na nadhani mimi ni mmoja wao, hivyo nina furaha sana kupewa jukumu hili, naweza kusema nimefarijika sana kupewa heshima kuwa ya kuifundisha klabu hii”.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.