Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kinda wa kitanzania Akram Afif ASAJILIWA VILLARREAL

Kinda wa kitanzania Akram Afif mwenye uraia wa Qatar amekuwa mchezaji wa kwanza kutoka Qatar kusajiliwa na klabu ya Hispania.

Mtoto huyo wa mchezaji wa zamani wa klabu ya Simba SC Hassan Afif amesajiliwa na Villarreal huku akionekana kuwa kuwa na kipaji cha hali ya juu kutoka taifa hilo la Mashariki ya Kati ambacho kitaisaidia klabu hiyo ya La Liga katika miaka michache ijayo.

Kijana uyo ambaye amezaliwa na kukulia mtaa wa Gerezani maeneo ya Kidongo chekundu jijini Dar es Salaam na kusoma shule zote za awali Tanzania, msimu huu alikuwa Ubeligiji akiitumikia klabu ya Eupen.

Afif ni zao la Aspire Academy inayomilikiwa na klabu ya Al-Sadd ambayo Raul Gonzalez aliitumikia kwa miaka miwili huku star wa Barca Xavi Hernández akiendelea kufurahia maisha yake ya soka.

Wale waliomfatilia kwa karibu mchezaji huyo mwenye miaka 19, wamekiri kwamba Afif anauwezo mkubwa wa kufanikiwa na miamba hiyo ya soka la Hispania na barani Ulaya. Mbali na kuwavutia ma-scout wa Villarreal, nyota huyo amevitoa udenda vilabu vingine vingi vya Hispania pamoja na klabu nyingine kama Porto na Zenit.

Afif hatakuwa na tatizo la lugha kwasababu tayari anauwezo wa kuzungumza Kispaniola kwani aliwahi kucheza kwenye academies za vilabu vya Villarreal na Sevilla kabla ya kuelekea Eupen kucheza ligi daraja la pili.

Katika kipindi alichocheza Kehrwegstadion, Afif alicheza mechi 17 na kufanikiwa kufunga magoli 6 kwenye ligi.

Tayari ameshafanya mazoezi na kikosi cha taifa cha Qatar na alifanikiwa kufunga goli kwenye ushindi wa magoli 15-0 dhidi ya Bhutan wakati timu hizo zilipokutana September 3, mwaka jana kwenye mchezo wa kuwania kufuzu kucheza fainali za kombe la dunia mwaka 2018.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.