Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kongamano la teknohama lasaka ubunifu TZ

Kongamano la teknohama lasaka ubunifu TZ

Teknohama na mawasiliano ni tasnia zinazokua kwa kasi sana Afrika Mashariki.
Nchi ya Tanzania ni mojawapo ya nchi ambazo zimewekeza takriban zaidi ya dola milioni 180 katika kupanua mkongo wa taifa.

Leo Kongamano la Sahara Spark linaloendelea jijini Dar es salaam,likiwa na maadhumuni ya kukuza ubunifu wa wanateknohama nchini hasa wanawake wanaoonekana kutoshiriki katika tasnia hiyo.

Kongamano la Sahara Sparks ni mkusanyiko wa vijana ambao ni wabunifu, wajasiriamali,serikali na wafadhili likiwa na lengo la kuona namna gani ubunifu na ujasiriamali vinaweza kutatua changamoto zinazokabili umma.

Caroline Ekyarisiima ni mwanzilishi wa taasisi ya 'apps and girls'.
Taasisi yake inawafundisha wasichana wa umri wa miaka 10 had 18 jinsi ya kutumia teknohama kutengeneza miradi ya kusaidia jamii zao.

Caroline ambaye alikuwa mwalimu wa sekondari anasema alianza na wasichana wachache lakini sasa anaona muamko wa wasichana wakitamani kujifunza zaidi.
 
                                          Baadhi ya ubunifu katika kongamano hilo
Caroline pia anasema ili kuendeleza sekta hiyo zaidi, serikali haina budi kupitia tena mfumo wa elimu na kuongeza masomo ya teknohama mapema kwa watoto.

Winnie ni mmoja wa wanafunzi waliopata mafunzo katika taasisi hio, akiwa na miaka 16 tu. Ametengeneza tovuti ya kukuza uelewa wa ugonjwa wa fistula pamoja na tovuti inayowawezesha wanafunzi kutoamalalamiko ya unyanyasaji na udhalalishaji wakiwa katika usafiri wa daladala.

Ubunifu wake umemshindia nafasi kwenye shule maarufu ya Africa Leadership Academy Afrika ya Kusini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.