Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kumbukumbu ya miaka 100 ya mapambano ya Verdun

Kumbukumbu ya miaka 100 ya mapambano ya Verdun

Viongozi wa Ujerumani na Ufaransa Jumapili (29.05.2016) wameshiriki kumbukumbu ya miaka 100 ya Mapambano ya Verdun kwa kuweka shada la maua katika makaburi ya wanajeshi 300,000 wa nchi hizo waliouwawa.
Mapambano ya Verdun ni mojawapo ya mapambano yaliochukuwa muda mrefu katika Vita Vikuu vya Kwanza vya Dunia ambapo yalidumu kwa siku 300 kuanzia Februari hadi Disemba mwaka 1916. Mapambano hayo kaskazini mashariki ya Ufaransa licha ya kuwa makali kabisa na kugharimu maisha ya wanajeshi 163,000 wa Ufaransa na wanajeshi 143,000 wa Ujerumani yalishindwa kutowa mshindi.

Miongoni mwa matukio ya mwanzo ya kumbukumbu hiyo viongozi hao wa Ujerumani na Ufaransa waliweka shada la mauwa katika makaburi ya wanajeshi wa Ujerumani huko Consenvoye kaskazini mwa mji wa Verdun ambapo miili ya wanajeshi wa Ujerumani ilizikwa.

Rais Francois Hollande wa Ufaransa na Kansela Angela Merkel wa Ujerumani walihudhuria hafla katika Ukumbi wa jiji huko Verdun ambapo katika hotuba yake Merkel amesema Verdun inasimamia sio tu "unyama usioelezeka na upuuzi wa vita " bali pia "kutowa mafunzo na usuluhishi wa Ujerumani na Ufaransa."

Mapambano ya Verdun ni funzo
Rais Francois Hollande wa Ufaransa na Kansela Angela Merkel wa Ujerumani. Rais Francois Hollande wa Ufaransa na Kansela Angela Merkel wa Ujerumani.
Amesema "ni wale tu wanaojuwa kipindi cha kale wanaweza kujifunza kutokana na hayo na kutumia jambo hili kujenga mustakbali mwema" na kuongeza kwamba dhana ya urafiki aliyoipata katika mji huo akiwa kama kansela wa Ujerumani "haifai kabisa kuchukuliwa kijuu juu".

Yeye na Hollande pia walimkabidhi Meya wa Verdun Tuzo ya mwaka huu ya Adenauer - de Gaulle ambayo hutunukiwa wale wanaochangia kujenga uhusiano mzuri kati ya Ujerumani na Ufaransa.
Hollande amesema Verdun sio kitu kilichoganda na mahala pa kutukuzwa kwa wafu bali daima imekuwa ikiangalia mbele kwa matumaini kutimiliza lengo lake la amani.
Watoto wa Ufaransa na Ujerumani takriban 3,400 wamepangiwa kuwasilisha mhadhara katika hafla ya kimataifa huko Douaumont ambapo miili ya wanajeshi 130,000 iliobakia kutoka pande zote mbili imezikwa.

Umuhimu wa Douaumont
Aliyekuwa Kansela wa Ujerumani magharibi Helmut Kohl na rais wa zamani wa Ufaransa Francois Mitterand wakiwa Verdun 1984. Aliyekuwa Kansela wa Ujerumani magharibi Helmut Kohl na rais wa zamani wa Ufaransa Francois Mitterand wakiwa Verdun 1984.

Makaburi ya Douaumont yana umuhimu wake kwani ni mahala ambapo Kansela wa Ujerumani magharibi wa wakati huo Helmut Kohl na aliyekuwa Rais wa Ufaransa Francois Mitterand waliposhikana mikono wakati wa kumbukumbu ya mwaka 1984 ya vita hivyo ikiwa ni ishara ya kihistoria ya usuluhishi kati ya mataifa hayo mawili.

Kumbukumbu ya mapambano hayo imekuja kuashiria uhusiano wa karibu uliopo kati ya Ufaransa na Ujerumani. Ni mwaka 1984 nchi hizo jirani ndipo zilipokubali kufanya hafla ya pamoja ya kumbukumbu ya mapambano ya Verdun ikiwa ni hatua nyengine mbele ya kukomesha uhasama na kutokuaminiana kati ya mataifa hayo mawili baada ya kumalizika kwa Vita Vikuu Viwili vya Dunia.
Mwaka huo pia ulishuhudia bunge la Ulaya likipitisha mkataba wa kuanzisha Umoja wa Ulaya na makubaliano kati ya Ufaransa na Ujerumani kuondowa ukaguzi wa mipaka hatua kwa hatua.

Changamoto kwa Umoja wa Ulaya
Wanafunzi wa Ufaransa katika warsha ya mapambano ya Verdun. Wanafunzi wa Ufaransa katika warsha ya mapambano ya Verdun.
Akizungumza katika mkesha wa kumbukumbu hii Kansela Merkel amesema ukweli kwamba amealikwa kuhudhuria kumbukumbu hiyo mwaka huu ni ishara jinsi uhusiano kati ya Ujerumani na Ufaransa ulivyo mzuri hivi sasa.

Ujerumani na Ufaransa zinaonekana kuwa engini kuu ya Umoja wa Ulaya unaoundwa na mataifa wanachama 28 ambao hivi sasa unakabiliwa na changamoto kubwa kama vile wimbi la wahamiaji na wakimbizi wanaokimbilia Ulaya na misukosuko ya kifedha inayozikumba baadhi ya nchi wanachama.

Uwezekano wa kujitowa kwa Uingereza kutoka umoja huo umezidi kuongezea hisia iliozagaa kwamba umoja wa kundi hilo uko hatarini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.