Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LEBRON AWEKA REKODI, CAVALIERS WATINGA FAINALI YA NBA.



LEBRON AWEKA REKODI, CAVALIERS WATINGA FAINALI YA NBA.



leb
Cleveland Cavaliers wamefanikiwa kutwaa ubingwa wao wa pili mfululizo kwa kanda ya Mashariki na sasa wanasubiri mshindi kati ya Golden State Warriors dhidi ya Oklahoma City Thunder ambao hata hivyo Thunder wanapewa nafasi kubwa kutokana na aina ya mchezo wanaoucheza sasa mpaka kufikia kuongoza 3-2.

Kwa LeBron James, hii ni mara ya sita mfuululizo kutinga Fainali ya NBA. Anakuwa mchezaji wa 8 kufanya hivyo katika historia ya NBA.

James alifunga pointi 33, Kevin Love alikuwa na pointi 20 na rebounds 12, na klabu ya Cavaliers ikatinga fainali yao ya pili mfululizo kwa kuichapa Toronto Raptors 113-87 katika mchezo wa sita wa fainali ya Mashariki iliyofanyika alfajiri ya Jumamosi.

Cavaliers itakuwa inataka kumaliza ukame wa miaka 52 wa kutokutwaa ubingwa wa NBA, ambao ni muda mrefu zaidi kwa mji wowote wenye timu angalau tatu za kimichezo. Hakuna timu inayotoka mji wa Cleveland ambayo imewahi kushinda taji lolote tangu Browns blanked Baltimore 27-0 kushinda NFL michuano ya mwaka 1964.

“Mji huu umekuwa na tamaa ya kutwaa ubingwa wa michuano hii,” alisema kocha Tyronn Lue. “Tuna timu nzuri na sahihi na tuna vipaji vizuri.”
James, ambaye alikulia katika mji jirani wa Akron, lazima anafahamu vyema ni kwa namna gani ubingwa wa michuano hii itakuwa na maana kubwa kwa mji wa Cleveland.

“Najua mji wetu unastahili kushinda ubingwa huu, mashabiki wetu wanastahili pia,” James alisema. “Lakini hiyo haitupi hisia ya kubweteka. Tumekuwa na bado tunatakiwa kutoka na kwenda kupambana. Bado tunatakiwa kutoka na kwenda kuchukua taji na kuthibitisha ubora wetu wenyewe.

Kyrie Irving alikuwa na pointi 30 na J.R. Smith aliongeza 15 kwa Cavaliers, ambayo inasubiri kukabiliana na mshindi wa fainali ya Magharibi kati ya Golden State-Oklahoma City ambayo imeingia mchezo wa sita na Thunder anaongoza 3-2.

Cleveland itaanza michezo yake nyumbani kama mabingwa wa Magharibi watakuwa Oklahoma City Thunder kutokana na rekodi zao za ushindi wa msimu huu lakini itaanza michezo yake ugenini kama itacheza dhidi ya Warriors waliokuwa na rekodi bora ya kushinda michezo 73.

Kyle Lowry alifunga pointi 35 na Demar DeRozan alikuwa na pointi 20. Raptors walishuhudia msimu wao bora kabisa katika historia ya klabu hiyo kwa kushinda michezo 56 huku pia wakishinda michezo yao ya mtoano mpaka fainali kwa mara ya kwanza. Mashabiki pia walihamasika na haikuwa ajabu kw atiketi zote 20,605 kuuzwa.

Katika kuonyesha wamefurahi kwa hatua ya timu yao ilipofikia muda wote walikuwa wakiimba kuiunga mkono hata katika dakika ambazo walionekana wasingeweza kurejea tena mchezoni.
Kocha wa Raptors Dwane Casey alisema kufikia mkutano fainali ilikuwa “ni hatua kubwa ya kujifunza na kuongeza uzoefu”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.