Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Marekani yaitaka UN kutumia nguvu kuwalinda raia

Marekani yaitaka UN kutumia nguvu kuwalinda raia

Marekani imeahidi kuunga mkono mpango wa kanuni kadhaa zinazowapa mamlaka wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na polisi kutumia nguvu ili kuwalinda raia katika migogoro ya kivita.
Mpango huo umeungwa mkono na Rwanda na Uholanzi. Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Samantha Power ametoa tangazo hilo katika mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa ulioangazia wajibu wa kuwalinda raia wanaokumbwa na machafuko, akisema kuwa Marekani “inajivunia” kujiunga na mataifa mengine 28 yaliyosaini mpango huo unaojulikana kana Kanuni za Kigali.

Walinda amani kutoka nchi 29 katika operesheni zilizoidhnishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwalinda raia sasa wanaruhusiwa kuchukua “hatua ya moja kwa moja ya kijeshi dhidi ya makundi yenye silaha yenye nia ya wazi ya kuwadhuru raia” – na makamanda wao wanaweza kuamuru matumizi ya nguvu “katika hali ya dharura” bila kushauriana na wakuu wao.

Power amesema Kanuni za Kigali zimetayarishwa kuhakikisha kuwa raia hawatelekezwi tena na jamii ya kimataifa, akirejelea namna walinda amani wa Umoja wa Mataifa walivyoondoka Rwanda kabla ya mauaji ya halaiki ya mwaka wa 1994 na Srebrenica kabla ya mauaji ya kinyama ya 1995.
Simon Adams, mkurugenzi mkuu wa Kituo cha Kimataifa cha Wajibu wa Kulinda, anasema 10 kati ya operesheni 16 za kulinda amani za Umoja wa Mataifa, ikiwemo asilimia 97 ya wanajeshi 105,000 na polisi wanaohudumu katika operesheni hizo, wana wajibu wa Baraza la Usalama kuwalinda raia.

Hata hivyo, licha ya kuwapo kwa operesheni za kulinda amani Umoja wa Mataifa unaendelea kupambana kuwalinda raia dhidi ya makosa mengi ya kikatili katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, Congo, Sudan na Sudan Kusini. Anaongeza Adams.

Power alisema nchi 29 ambazo zimeidhinisha Kanuni za Kigali zinajumuisha zaidi ya wanajeshi 40,000 wa Umoja wa Mataifa na polisi, ikiwa ni zaidi ya thuluthi moja ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa. Umoja wa Mataifa ndio mchangiaji mkubwa wa kifedha kwa operesheni za kulinda amani za umoja huo lakini una wanajeshi wachache mno wanaotumwa katika operesheni zake.

Rwanda, Uholanzi na Marekani ziliuanzisha mpango huo wa msingi ambao uliidhinishwa katika mkutano wa ngazi ya juu mnamo Mei 2015 mjini Kigali na mataifa makuu 30 yanayochangia wanajeshi na polisi kwa operesheni za Umoja wa Mataifa, wachangiaji kumi wakuu wa kifedha namataifa mengine.

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Uholanzi Bert Koenders aliumbia mkutano huo kuwa watu na jamii zilizoko chini ya kitisho, bila mahali pa kwenda, zinapaswa kujua kuwa Umoja wa Mataifa utafanya kila liwezekanalo ndani ya uwezo wake kuwapa ulinzi.

Balozi wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa Eugine-Richard Gasana alisema kanuni hizo zinaleta operesheni za kulinda amani “katika karne ya 21”. Amesema zaidi ya wanajeshi 6,000 wa Rwanda katika operesheni za kulinda amani za Umoja wa Mataifa wamepewa mafunzo ya kuzingatia kanuni hizo na “wamejiandaa kutumia nguvu ikiwa watahitajika” kwa ajili ya kuwalinda raia.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.