Messi kizimbani kwa kukwepa kulipa kodi
Nyota wa Argentina Lionel Messi, mmoja wa wanamichezo wanaolipwa pesa
nyingi zaidi duniani, anafikishwa kizimbani kesho mjini Barcelona kwa
tuhuma za kuipunja Uhispania kwa kukwepa kulipa kodi za kiasi cha euro
milioni 4
Baada ya kuisaidia Barcelona kushinda mataji mawili msimu uliokamilika, La liga na Kombe la Mfalme, mshindi huyo mara tano wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa mwaka na babake Jorge Horacio Messi watafikishwa mahakamani kuhusiana na kesi hiyo ambayo imemwandama tangu Juni 2013.
Kesi hiyo itaendeshwa hadi Juni 2 – siku ambayo Messi anatarajiwa kutoa ushahidi pamoja na babake.
Vikao vya mahakama vinakuja siku chache tu kabla ya kujiunga na wachezaji wenzake wa Argentina kushiriki katika kinyang'anyiro cha Kombe la Mataifa ya Amerika Kusini, maarufu kama Copa Amerika litakaloandaliwa Marekani.
Maoni
Chapisha Maoni