Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mfahamu mmiliki mpya wa Aston Villa Tony Xia toka China


Mfahamu mmiliki mpya wa Aston Villa Tony Xia toka China


Mfahamu Dr Tony Xia ambaye ndiye meneja mpya wa klabu ya Aston villa kuhusu uzoefu wake katika masuala ya michezo na ni kipi anatarajia kuifanyia klabu hiyo aliyoinunua. Dr Xia ameahidi kurejesha mpira wa Uingereza katiba klabu hiyo ambayo yeye ndiye atakuwa kiongozi mkuu.
Japokuwa Dr Tony Xia ni miongoni mwa watu wenye fedha duniani, lakini si mtu anayefahamika sana. Historia yake katika mpira, chanzo cha fedha zake na vingine vingi ni wachache sana wanavifahamu.
Hapa tunakuwezesha wewe kufahamu mmiliki mpya wa klabu ya Asto Villa.
Dr Tony Xia ni nani?
Tony Xia alizaliwa katika Mji wa Quzhou ambao uko umbali wa maili 250 kusini magharibi mwa Shanghai. Baba yake alikuwa ni mkulima na mama yake alikuwa ni mama wa nyumbani. Kutokana na uwezo wake mzuri aliouonyesha darasani, alienda Marekani kusoma katika Chuo Kikuu cha Havard na MIT na wakati huo huo akichukua kozi ya miezi 5 katika Chuo cha Oxford.
Ametoa wapi uwezo wa kununua Aston Villa?
Bado haijafahamika kiasi halisi cha utajiri anachomiliki lakini huwezi  kuacha kumuweka katika kundi la mabilionea. Anamiliki moja ya kampuni kubwa ambayo imeajiri takribani watu 35,000 katika nchi 75. Recon Group ni moja ya makampuni ya kimataifa, ni kampuni hii hujishughulisha na mambo mengi ikiwa ni pamoja na Information Technology (IT), Afya, Uhandisi, Usafrishaji na Michezo.
Ameinunua klabu ya hiyo kwa kiasi cha Euro milioni 60, lakini fedha hizo zitapanda na kufika Euro milioni 100 kama klabu hiyo itafanikiwa kupanda daraja. Huu ni moja kati ya uwekezaji mkubwa kufanyika katika ukanda wa China.
Je! anauzoefu gani katika masuala ya mpira?
Xia alikuwa akisakata kabumbu hadi alipomaliza chuo na pia amekuwa akitamani sana kumilikia klabu ya mpira na kuisaidia China kukua kimpira kama ndoto za Rais wa nchi hiyo zilivyo. Rais wa China ni rafiki karibu wa Tony Xia na kunauwezekano msimu ujao akazuru Villa Park.
Xia aliangalia baadhi ya klabu ikiwemo Everton, lakini alipohudhuria mchezo wa mwisho wa Aston Villa alivutiwa na mwamko wa mashabiki wa timu hiyo akaamua kuinunua.
Sasa mashabiki wa Aston Villa wategemee nini?
Tony Xia anatarajia kuweka fedha za kutosha mezani ili kuweza kuwapandisha Aston Villa daraja hadi ligi kuu.  Inasemekana kuwa anatarajiwa kutoa kiasi cha euro milioni 40 huku akiwa kwenye mchakat wa kumtafuta kocha atakaye kinoa kikosi hicho. Kati ya makocha wanaopewa nafasi kutua Villa Park ni pamoja na Roberto Di Matteo ambaye ana nafasi kubwa zaidi na Nigel Pearson.
345DB86200000578-3599063-image-a-86_1463667622593Roberto Di Matteo
Steven Hollis ambaye ndiye mwenyekiti aliyeachia madaraka baada ya kuja kwa Tony Xia amesema kuwa inafurahisha kumuona mtu kama yeye kuimiliki klabu kwani inaonekana kuwa anakitu anachotamani kufanikiwa, hivyo ukiweka wachezaji wanaotamani kufanikiwa, pamoja na tamaa yake ya kufanikiwa hakika unajenga kitu kikubwa ambacho kitaonekana siku za karibuni.
3458EE3600000578-3599063-image-m-88_1463667805515Randy Lerner aliyekuwa mmiliki wa Aston Villa.
Aidha amewataka mashabiki wa klabu hiyo kumuunga mkono Tony Xia kwani anakwenda kufanya jambo kubwa na watalifurahia.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.