Ruka hadi kwenye maudhui makuu

mwanaume mwenye mvuto zaidi kwa wanawake

Sayansi imethibitisha mwanaume akiwa na sifa hizi 10 huwa na mvuto zaidi kwa wanawake

Kama wewe ni mwanaume na una sifa hizi, basi fahamu kuwa sayansi imethibitisha kuwa una mvuto kwa wanawake
7-ways-to-let-him-know-your-interested-3
1. Sura Nzuri
Muonekano mzuri kwa mwanaume huwa ni kigezo cha kwanza katika maamuzi ya mwanzo kwa mwanamke lakini hata hivyo huwa ni katika mapenzi ya muda mfupi tu zaidi ya yale yanayodumu.
2. Ucheshi
Ucheshi kwa mwanaume si muhimu tu kama wenyewe bali humfanya mwanaume aonekane mwenye akili

3. Mwanaume anayetoa msaada

Wanawake hupenda wanaume wanaotoa msaada, wasio wachoyo pale wanapotafuta uhusiano wa muda mrefu

4. Utajiri/Uwezo wa kifedha

Ile imani kuwa wanaume wenye uwezo wana mvuto zaidi kwa wanawake ni kweli. Utafiti ulionesha kuwa wanawake huona wanaume wanavutia zaidi pale wanaposimama tu kwenye magari ya kifahari au nyumba, hata kama vikiwa sio vyao.
5. Umri Mkubwa
Wanawake hupenda wanaume wenye umri mkubwa kwasababu mara zote huamini kuwa wamekusanya vitu vingi na uzoefu katika maisha.
6. Ndevu
Ndevu zimekuwa zikichukuliwa kama zinazokera na kuvutia kwa wakati mmoja – yote hutegemea na mapenzi ya mtu.
7. Wagumu
Wakati utafiti wa zamani unasema kuwa wanawake huvutiwa na wanaume wanawaopenda, tafiti mpya zimedai kuwa kujifanya mgumu, kutojali kunawavutia wanawake. Kifupi, wanaweza kutaka kile wanachodhani hawawezi kupata.
8. Tafiti zinaonesha pia kuwa wanaume wenye mbwa huwavutia wanawake. Duh!
9. Wanawake kwenye tamaduni zote wameonesha kuvutiwa na wanaume wanaovaa rangi nyekundu
10. Wanawake wamethibitishwa pia kuwapenda wanaume majasiri na wasiogopa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.