Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NCHI TAJIRI ZAIDI BARANI AFRIKA

Ukisema uingie mtaani sasa hivi kumuuliza mtu mmojammoja ni nchi ipi tajiri zaidi Afrika huenda ukapata majibu tofauti lakini uhakika wa hilo upo kwenye ripoti mpya iliyofanywa kwa bara la Afrika.
Nigeria ni nchi ambayo Dunia inajua kuhusu mafuta yao, inajulikana pia majina ya matajiri wao kama akina Alhaji Aliko Dangote.. mengine yanayosikika sana kutoka huko ni ishu kama za mashambulio ya Kigaidi, leo imeingia kwenye headlines nyingine.
Utafiti uliofanyika umekuja na majibu tayari, Nigeria ndio nchi inayoongoza kwa utajiri sasahivi ndani ya Afrika… South Africa iko nafasi ya pili alafu zinafuatia nchi nyingine.
Ninayo list ya Top 10 ya nchi zote hapa.
No.1: Nigeria, hii ina sifa nyingine kubwa kuwa nchi inayoongoza kwa kuwa na watu wengi zaidi Afrika, na pia utajiri wake unatokana sana na uzalishaji wa mafuta.
No.2: South Africa, sehemu kubwa ya Utajiri wao inatokana na uchimbaji wa madini.
No.3: Misri
No.4: Algeria, nao wako kwenye list ya wauzaji wakubwa wa mafuta na gesi.
No.5: Morocco, uwekezaji wao mkubwa uko kwenye Utalii, viwanda vya nguo na Kilimo.
No.6: Sudan.. sio rahisi kukutana na nguo imeandikwa ‘Made in Sudan’, lakini wao ni wauzaji wakubwa sana wa pamba duniani.
No.7: Kenya, biashara yao kubwa ni chai na kahawa.. sikuwahi kujua kumbe hata biashara ya kuuza maua kwenda Ulaya nayo ni biashara inayoingiza pesa nyingi Kenya.
No.8: Angola.. japo walipitia kipindi kigumu cha vita kwa zaidi ya miaka 25, bado madini, mafuta na kilimo vimeiweka nchi hiyo ndani ya Top 10 ya nchi tajiri Afrika.
No.9: Libya.. Hii ndio nchi ya kwanza Afrika ambayo wataalam wamesema kuwa ina akiba kubwa ya mafuta ndani ya Afrika mpaka sasa, na hiyo ndio inayoiingizia nchi hiyo pesa nyingi zaidi kila siku.
No.10: Tunisia.. wao biashara yao kubwa ni spare za magari, kuuza mafuta na utalii.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.