Ozil: Hili Ndilo Tatizo kuu la Arsenal
Mesut Ozil amebainisha kile anachoamini kilikuwa
sababu ya Arsenal kushindwa kutwaa taji la Ligi Kuu Uingereza msimu huu,
unataka kukijua?
Lakini baada ya kusalimu amri na kuiachia Leicester City ubingwa, Ozil ambaye amefanikiwa kutoa pasi 19 za goli katika ligi, amekiri kwamba kiwango cha Arsenal mwezi Machi pamoja na idadi ya majeruhi ndizo sababu zilizowanyima ubingwa.
"Nadhani tulipoteza pointi nyingi ambazo tulitakiwa kushinda dhidi ya vitimu vidogo, hasa baada ya mechi za Barcelona" Mjerumani huyo alisema.
Tofauti na kucheza chini ya kiwango, kiungo huyo anaamini Arsene Wenger atahitaji kuimarisha kikosi kwa kuongeza wachezaji thabiti na wenye nguvu majira ya joto.
"Mambo mengi ni lazima yarekebishwe, mojawapo ni majeruhi; tunahitaji kusajili zaidi wachezaji wenye nguvu" aliongeza Ozil.
"Tutakuwa imara zaidi ya msimu uliopita. Wachezaji wapya wataifanya timu kuwa imara zaidi."

Maoni
Chapisha Maoni