Picha zikionyesha matukio mbalimbali toka Bungeni- Dodoma
Wabunge wakiondoka ndani ya Ukumbi wa Bunge mara baada ya Naibu Spika kutangaza kuahirisha shughuli za Bunge leo.
Baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri wakifuatilia masuala
mbalimbali ndani ya Ukumbi wa Bunge wakati wa kikao cha 32 cha Bunge
hilo mjini Dodoma
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla akijibu maswali ya wabunge kuhusu sekta ya
Afya Bungeni mjini Dodoma.
Mbunge wa jimbo la Ukonga (CHADEMA) Mhe. Mwita Mwikwabwe akisoma kitabu cha Kanuni za Kudumu za Bunge ndani ya Ukumbi wa Bunge.
Mbunge wa Nzega Mhe. Hussein Bashe (CCM) akizungumza jambo
na Mbunge wa Arumeru Mashariki (CHADEMA) Mhe. Joshua Nassari (kulia)
nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao cha 32 cha
mkutano wa tatu wa Bunge leo mjini Dodoma.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari
Barbro Johansson iliyoko jijini Dar es salaam wakiondoka ndani ya ukumbi
wa Bunge mjini Dodoma mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali
na majibu.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Sulemani Jafo akijibu maswali ya wabunge
yaliyoelekezwa kwenye wizara yake Bungeni mjini Dodoma.
Wabunge wa Chama cha Mapinduzi
(CCM) wakiwa wamesimama ndani ya ukumbi wa Bunge kufuatia Naibu Spika wa
Bunge hilo Mhe. Tulia Ackson kutangaza kuliahirisha Bunge leo mjini
Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akizungumza
jambo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Kikanda na Kimataifa Dkt. Suzan Kolimba nje ukumbi wa Bunge.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Thomas Kashililah (kulia) akizungumza jambo na wabunge leo mjini Dodoma.
Mbunge wa Arumeru Mashariki
(CHADEMA) Mhe. Joshua Nassari (kushoto) akisisitiza jambo kwa Mwenyekiti
wa Bunge Mhe. Andrew Chenge ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Magharibi
nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.
Mbunge wa Kigoma Mhe. Peter Selukamba akijadiliana jambo
na Mbunge wa Nzega mjini Mhe. Hussein Bashe (kushoto)Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu nje ya Ukumbi
wa Bunge mjini.
Kikao cha 32 cha Mkutano wa 3 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asubuhi.
Mbunge wa Arumeru Mashariki (CHADEMA) Mhe. Joshua Nassari
(kushoto) akimweleza jambo Mwenyekiti wa Bunge Mhe. Andrew Chenge ambaye
pia ni Mbunge wa Bariadi Magharibi nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.
PICHA/Aron Msigwa na Fatma Salum – DODOMA
Maoni
Chapisha Maoni