Mchezaji aliyetekwa aokolewa na polisi Mexico
Polisi ya Mexico imemwokoa mchezaji wa kandanda aliyetekwa nyara Alan Pulido, ambaye ameonyeshwa leo katika kikao kifupi cha wanahabari akitangaza kuwa yuko katika hali nzuri.Polisi na maafisa wengine walisema Pulido, mshambuliaji mwenye umri wa miaka 25 anayechezea klabu ya Ugiriki ya Olympiakos, aliokolewa katika operesheni ya usalama iliyokamilika usiku wa manane katika mji wa mpakani wa kaskazini mashariki wa Tamaulipas. Pulido alichukuliwa na watu waliokuwa na silaha Jumamosi usiku wakati akirejea nyumbani kutoka kwenye tafrija.
Pulido, aliyekuwa katika kikosi cha Mexico kilichocheza Kombe la Dunia mwaka wa 2014 nchini Brazil, alitekwa nyara nje ya mji aliozaliwa wa Ciudad Victoria. Maelfu ya watu hutekwa nyara nchini Mexico kila mwaka, mara nyingi na magenge yanayohusika na ulanguzi wa dawa za kulevya
Maoni
Chapisha Maoni