Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Sababu mbili kwanini Koffi Olomide hakuhudhuria mazishi ya Papa Wemba

Sababu mbili kwanini Koffi Olomide hakuhudhuria mazishi ya Papa Wemba

Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Dunia kwa ujumla siku za hivi karubini zilikumbwa na huzuni baada ya kumpoteza nguli wa muziki wa miondoko ya Rhumba Papa Wemba. Siku chache baada ya kifo chake alizikwa katika Mji wa Kinshasa DRC na mazishi yake kuhudhuriwa na watu wengi.

Kikubwa kilichowashangaza watu wengi ni Mwanamuziki mwenzake Antoine Christophe Agbepa Mumba maarufu kama Koffi Olomide kutohudhuria mazishi ya Papa Wemba. Sasa imefahamika kuwa kuna sababu kuu mbili kwanini Koffi Olomide hakuonekana kwenye msiba wa Papa Wemba.
  1. Papa Wemba alishwahi kusema enzi za uhai wake kuwa akifariki Koffi Olomide asihudhurie mazishi yake. Inasemekana kuwa wasanii hawa hawakuwa na mahusiano mazuri. Itakumbukwa kuwa Papa Wemba alimsaidia sana Koffi Olomide kumkuza kimuziki wakati wakiwa wote katika bendi ya Viva La Music.
2. Sababu ya pili ni kuwa, siku kadhaa baada ya Papa Wemba kufariki, Charles Agbepa ambaye ni baba mzazi wa Koffi Olomide alifariki nchini Ufaransa. Hivyo hakuweza kuhudhuria msiba wa Papa Wemba kutokana na kifo cha baba yake.
Source- Kivu Media

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.