Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Shilole na Vanessa tusahau yaliyopita tugange yajayo

Usiku wa Jumanne ulikuwa ni wa furaha kwa wale wasiopenda maendeleo kwani walitumia msemo “vita vya panzi furaha ya kunguru” baada ya Shilole na Vanessa kutupiana maneno ya kukashifiana na kutishiana wakati kila mmoja akijua dhahiri hilo ni kosa kisheria.

“Vee Jipange sana mwenzio Igunga niliaga sijaletwa kwa kubebwa kwenye lori, nimekuja na mbio za mwenge,” aliandika Shilole kwenye post ya Instagram ambayo imefutwa tayari. “We si wa magorofani na kiingereza chako cha kuunga, mi ndio mtoto wa mbwa sasa maninaa,” aliandika Shilole.

Vanessa alijibu kwa kuandika: “ Nikupe Kickiii ujulikane au sio? Kila siku twanyamaza ndio mtugaraze. Sit the f*ck down. Mimi sio wale uliowazoea. Ps: You ain’t worth this post inashushwa sasa hivi #MessageSent.”

Sitaki kuamini kuwa kilichokuwa kimefanyika ni kutafuta kiki kwa wanadada hao ya wimbo ‘Say My Name’ wa Shilole na kuandaa mazingira ya albamu mpya ya Vanessa ‘Money Monday’ ambayo amepanga kuiachia mwaka huu japo muda haujajulikana.

Shilole alimuonya Vanessa kwa kupost kipande cha video kilichokuwa na baaddi ya maneno yaliyosema, “Listen to me my sister, you see me nah, mimi mwenzio nimezaliwa Igunga, nimezoea kula ugali, sijazoea kula chips mayai kama unavyokula wewe. So mama ninapiga kuliko maelezo, usiombe kukutana na mimi, au waulize wenzio waliokutana na vibao vyangu wanaweza kukuambia kwamba kibao cha Shishi ukikutana nacho lazima uombe Panadol.”

Funika kombe mwanaharamu apite, lakini Vanessa hakutaka kujua hilo alijibu mapigo kwa kutuma kipande cha video na yeye kwa kusema, “But look, there is now way, there is no time, it’s too much effort to try lower a little myself and what I stand for your nonsense, kama huelewi chukua time na vimaneno vyako viwili vya Kiingereza.”

Kwanini hiyo nguvu ya kutishiana na kutupiana maneno ya kejeli mitandaoni msingetumia kutafuta vipaji vya wasanii wengine wa kike wakati munajua wasanii wa kike bongo mpo wachache na mnao kick hamzidi watano?
Vanessa unaonekana umetoboa Afrika nategemea kuona makubwa kwako lakini kwa hiki kilichotokea umeniangusha. Napenda kusikiliza nyimbo yako ya ‘Hawajui’ kwanini usijifunze kutokana na mashairi yako uje kuwa Queen of Africa kutokea bongo.

Napenda kuona tena Shilole na Vanessa wakipeana support kwenye vitu vya maana na kushikana mikono kuupanua muziki wetu kwa kuwaonyesha watu wa nje kuwa bongo tuna wasanii wa kike pia wanaofanya vizuri siyo kina Alikiba, Diamond, AY, Joh Makini pekee.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.