Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tabia 8 za wazazi ambazo huenda zikawafanya watoto wasifanikiwe vizuri kimaisha

Tabia 8 za wazazi ambazo huenda zikawafanya watoto wasifanikiwe vizuri kimaisha

Kuzaa sio kazi, kazi kulea mwana, waswahili walisema. Kama mzazi ni jukumu lako kuhakikisha mwanao anakua katika mazingira mazuri na elekezi kwakwe kumfanya awe ni mwenye hekima kuanzia mdogo mpaka katika utu uzima wake.
Kulea ni kazi, tena asikuambie mtu ni kazi kubwa sana kulikoni hata ya kubeba zege. Kumkuza mtoto mdogo awe vile unavyotaka kupitia muonekano wako au mtazamo wako ni kitu kikubwa sana na kama unajiona uko hivyo ulivyo sasa kwa sababu ya wazazi wako washukuru. Maana si kazi ndogo waliofanya.
Kuna vitu kadha wa kadha ambavyo vinaweza kuchangia katika ukuaji au malezi kwa namna moja au nyingine. Mfano mazingira unayoishi, hali ya kijamii na uchumi wa familia, na vile vile elimu ya wazazi wanaomlea mtoto.
Ni vigumu kujua njia ipi ya malezi itakuwa sahihi, ila kuna tabia za wazazi za aina Fulani ambazo wanasayansi wamegundua inaweza kuathiri malezi ya mtoto kwa njia chanya ama hasi.
Zifuatazo ni tabia ambazo wazazi wengi wanazo ambazo hupelekea watoto wao wasifanikiwe maishani.
  1. Wazazi wasio wahamasisha watoto wao kujitegemea/ kuwa huru.
Wazazi wanashauriwa kuwahimiza watoto wao kuwa wenye kujitegemea kimawazo na kujiamini, hii inasaidia sana hata anapokutana na vishawishi katika rika lake, ajue lipi baya lipi zuri. Unapomwamulia kila kitu haumjengi, unamjenga mtoto endapo utamfanya ajiamini na kujitegemea. Kumbuka kwamba hautaishi nae milele, jifunze sasa kumwacha huru katika maamuzi madogo atajiamini kutatua matatizo yake binafsi
2. Wazazi wanaokaripia watoto wao mara kwa mara.
Unapokuwa unatumia maneno makali makali kila mara mtoto awapo amekosea kuna madhara ya muda mrefu. Kumkaripia mtoto, kumtukana, kumsema kwa kejeli humfanya mtoto awe kwanza muoga wa kila kitu au tuseme si mthubutu, hii peke yake imtarudisha nyuma katika makuzi yake na vile vile kama mzazi, jaribu kutafuta njia mbadala ya kumfunza mtoto maana kuna usemi unasema ‘mtoto umleavyo ndivyo akuavyo’, mtaanza kufokeana ndani ya nyumba akifikia umri wa balehe na kumbe lilikua kosa lako.
3. Tabia ya mzazi utaka kujua kila kitu kinachoendelea katika maisha ya mtoto.
 Sawa ni kitu kizuri kwa upande mwingine, unakua haukosei sehemu yoyote ya maisha ya mwanao lakini kuendesha kila kitu chake kutampelekea mtoto awe na wasiwasi na huzuni kupindukia. Hawezi kufanya uamuzi wowote ule katika maisha yake bila wewe kuwepo, unakuta mama au baba walitaka kuwa madaktari ikashindikana, wanalazimisha sasa ndoto zao zitimizwe na mtoto na yeye kwa uoga wa kuwasaliti anang’ang’ania fani ambayo wala haiwezi maskini, ni lazima tu atafeli, tena sio shule tu, anafeli hadi maisha. Maana muda wake mwingi anautumia kufanya kitu ambacho hakina manufaa kwake kwasababu tu mzazi alisema.
  1. Kumuacha mtoto aamue mwenyewe muda wa kulala.
 Wenzetu wazungu ndio wanalifatilia sana, lakini ni kitu kimoja muhimu sana, ukuaji wa ubongo wa mtoto mdogo wanasayansi wanasema unahitaji fomula, mtoto hawezi kuamua mwenyewe alale saa mbili usiku kila siku, leo atalala saa moja kama alichoka sana, kesho atalala saa 3 kama kwenye TV kulikua na kipindi anachopenda kukiangalia, na siku nyingine atalala hata saa sita ukiamua umuache mwenyewe aamue. Mpangie muda wa kulala usiopungua masaa 9-10 usiku hili litamsaidia hata akiamka kuwa mwenye nguvu za kujifunza vitu vipya na ubongo wake utakua kwa nafasi.
  1. Kumuacha mtoto angaalie TV akiwa mdogo sana. 
Watoto wanaongalia TV wakiwa na umri chini ya miaka 3 huathirika sana katika jinsi wanavyoongea, au kushiriki na watoto wengine. Tunaweza ona kwa sasa ni njia rahisi ya kulea maana unamwacha anakodolea TV hapo we unaendelea na kazi nyingine, la hasha, hilo liache mapema sana, TV inaonyesha mengi, vurugu, lugha za matusi, picha zisizofaa kwa watoto yote haya yanaingia kwenye kichwa chake na kuanza kujenga tabia ambazo atakua nazo, na najua tu hatutazipenda. Jaribu kusomea vitabu, una kazi zimekubana amezoea vitabu atafunua vitabu vyake ataangalia picha akishindwa atacheza na toys zake. Ana muda mwingi sana wa kuja kuangalia TV badae.
  1. Wazazi wanaotumia mabavu:
 Mzazi anayetumia mabavu ni yule anayetoa amri moja, na usipoifata utaona cha mtema kuni, mfano anaposema ‘ufaulu mtihani la sivyo ukifeli usirudi nyumbani’ . Kwa wakati mwingine mzazi mwenye mamlaka na mwenye kutaka aeleweke kwanini amesema hivyo ujumbe wake utatoka kwa namna tofauti, mfano ‘inakulazimu ufaulu mtihani, maana watu wote walifanya vizuri mashuleni wana maisha mazuri baada ya shule’. Hawa ni wazazi wawili tofauti. Ulezi wa kutumia mabavu haujengi hata kidogo, sasa kwa mfano mtoto kafeli ndio, alafu harudi nyumbani si ataishia kuwa mtoto wa mtaani, au kibaya zaidi kuwa kibaka.
  1. Kutokuwa karibu na mtoto au kutokumpa mapenzi mtoto.
Hakuna kinachoweza kuwa badala ya mapenzi au uwepo wako kwa mtoto wako, tena hii ni kiafya na makuzi ya kawaida. Tengeneza ukaribu na mwanao, mpe mapenzi aone kama kweli duniani wazazi ndio wanatufunza mapenzi. Watu wengi wanamatatizo ya kutokuamini watu, au kutokufungua hisia zao na kuruhusu kupendwa kwa vile tu wazazi wake hawakumfanya aone ni kawaida kuachia moyo huru ukapenda au kupendwa.
Na vile vile kumpongeza mtoto wako anapofanya vizuri, au kumwambia/kumuonyesha mwanao unampenda ni muhimu katika makuzi ya mtoto mdogo, kwanza halikupunguzi kitu, bali linakuongezea ukaribu na mwanao.
  1. Wazazi wanaotumia fimbo kumuelimisha au kumfunza mtoto
Fimbo au vibao havijawahi kuwa njia mathubuti ya kumfunzia mtoto, kwa upande mwingine kwanza unakuwa umezidiwa busara na mtoto mdogo mpaka unapandwa na hasira za kuchapa. Kama wewe uko hivyo, unategemea yeye atakuja kuwa vipi? Si ndo wa kushikana mashati na wenzie mtaani?. Uchunguzi unasema, kumchapa mtoto hakumfunzi, bali kunamfanya awe sugu na badae watoto hawa huishia kuwa mazezeta na wenye kushindwa kujitambua.
Wewe kama mzazi una nafasi kubwa ya kuamua namna mtoto wako atakavyokuja kuwa baadae. Kumbuka “Samaki mkunje angali mbichi,” “Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.