Uingereza kuwapa wafungwa iPads waweze kuwasiliana na familia zao
Imependekezwa kwamba, wafungwa wapewe iPads ili iweze kuwasaidia kuongea moja kwa moja na familia zao. Pendekezo hili linalotarajiwa kukamilishwa na Michael Gove, ambae ni Katibu wa Sheria nchini humu na vile vile ni mbunge kutoka Surrey Heath
Uchunguzi uliofanywa na The Guardian katika elimu ya gerezani, ndio ulitoa mapendekezo haya ya matumizi makubwa ya teknolojia kwa wafungwa ili waweze kujiendeleza wenye.
Vile vile mapendekezo mengine yanayotarajiwa kuafikiwa ni ya wafungwa kufungwa tags ambazo zitatumika kama vitambulisho na zitakuwa zikifuatiliwa na satelaiti. Kwa hili pendekezo inamaanisha kwamba wafungwa (wahalifu) watapunguza muda wa kuwa gerezani. Na kwa wale wasio na makosa makubwa na ni wafanyakazi, itawapasa kutumikia kifungo chao wakati wa mwisho wa wiki. Na muda mwingi wote wanatakiwa kuwa maeneo yao ya kazi. Yote hiyo itawezekana kwa wao kuvalishwa hizo tags (vitambulisho) zitakazokua zinafatiliwa na sateliti.
Maelfu ya wafungwa wengine ambao watakua wanakaribia mwisho wa kutumikia kifungo chao, wataruhusiwa muda wa mchana kuenda sehemu watakazo pangiwa kufanya kazi ili waanze kufanya kazi mapema.
Mahakama itatakiwa kutumia sana adhabu yake ya kufanya kazi za kijamii kama njia mbadala ya kuwapeleka watuhumiwa jela.
David Cameroon alisikika akisema, kwa muda mwingi tumeacha magereza yetu yawe imara, sio tu kwamba inaongeza mzungo wa uhalifu, bali pia inaongeza bili kwa walipa kodi ambazo zinaenda kwa watu walishindikana katika jamii, na hakuna sehemu nyingi ambapo wangeweza kubadilishwa zaidi ya humo humo kwenye magereza yetu. Hivyo basi Jela haitakua tena sehemu ya wafungwa kupumzika, bali itakua sehemu ambayo maisha ya watu wengi yatabadilika’.
Katibu wa Sheria Michael Gove naye alisema, ‘Gereza ni lazima litoe mafunzo zaidi kwa wahalifu, tutawaweka magavana kwenye madaraka, waweze kuwa huru kuamua jinsi ya kuendesha magereza haya jinsi wao wanavyodhani ni sahihi.
Maoni
Chapisha Maoni