Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Vurugu ndani ya Bunge za sababisha Zitto, Mdee, Lissu kusimamishwa kuingia Bungeni

Vurugu ndani ya Bunge za sababisha Zitto, Mdee, Lissu kusimamishwa kuingia Bungeni


Kufuatia mvutano mkali uliotokea lengo bungeni, adhabu kali zimetolewa kwa wabunge wa upinzani ikidaiwa kuwa ni kukiuka maadili ya bunge hilo. Baadhi ya wabunge walioonywa na kupewa adhabu ni pamoja na
Wabunge wote wa Upinzani wamepewa onyo kali kwa kung’ang’ania Bunge lionyeshwe moja kwa moja na na kituo cha televisheni ya Taifa (TBC).

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu na na Mbunge wa Bunda Esther Bulaya wamesimamishwa kwa mikutano 2 ya Bunge. Hivyo wabunge hawa hawataingia bungeni hadi mwakani 2017.

Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe na Mbunge wa Kawe Halima Mdee wamesimamishwa shughuli za Bunge mpaka mwezi Septemba 2016.

Wabunge wengine waliofungiwa ni pamoja na Mbunge wa Babati Mjini Pauline Gekul, Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, wamefungiwa kushiriki vikao vilivyobaki vya bajeti. Kwa upande wa Mbunge wa Tarime John Heche, yeye amefungiwa kuhudhuria vikao kumi mfululizo vya bajeti kuanzia leo.

Huu ni uamuzi wa kamati Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge chini Mh George Mkuchika (Mb)
Aidha wabunge wa Upinzani wametoa Hoja ya kutokuwa na Imani na Naibu Spika kwa mujibu wa kanuni ya 138(1) ya Bunge na Ibara ya 85(4)(c) ya Katiba.

Kwa upande wa wabunge wa CCM, akizungumza mbunge Joseph Msukuma ambaye ni mbunge wa jimbo la Geita Vijijini amesema kuwa kusimamishwa kwa wabunge wa upinzani ni fundisho kwa wabunge wengine.

Mbunge wa Ulanga Goodluck Mlinga (CCM) yeye amesema kuwa kusimamishwa kwa wabunge ni kwamba ni kujenga heshima kwa Bunge. Aidha ametaka hili liwe fundisho kwa wabunge waliobaki na anaunga mkono hoja kusimamishwa kwao

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.