Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga mabingwa wa kihistoria VPL

BINGWA WA KIHISTORIA VPL

Yanga imekabidhiwa taji lao la ubingwa wa VPL msimu wa 2015-16 baada ya kufanikiwa kulitetea taji hilo ambalo walilitwaa msimu uliopita. Yanga imepewa kombe hilo ikiwa na pointi 74 huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi baada ya kutoka sare na Ndanda FC kwenye uwanja wa taifa.

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mchezo huo alilikabidhi kombe hilo kwa nahodha wa Yanga Nadir Haroub ‘Cannavaro’ baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Ndanda FC dhidi ya Yanga.

Ubingwa huo unawafanya Azam FC kulikosa taji hilo ndani ya misimu miwili mfululizo wakati Simba wao wameendelea kulikosa taji hilo ndani ya misimu minne mfululizo.

Mambo muhimu kufahamu
  • Yanga wametwaa ubingwa wao wa ligi kuu ya soka Tanzania bara kwa mara ya 26 kwenye historia ya klabu hiyo
  • Ubingwa wa msimu huu ni wa pili mfululizo baada ya kuunyakua msimu uliopita na kufanikiwa kuutetea kwa mara nyingine.
  •  Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amenyanyua kombe hilo kwa mara ya pili akiwa kama nahodha wa kikosi cha Yanga. Msimu uliopita, Cannavaro alinyanyua ndoo hiyo kwa mara ya kwanza akiwa nahodha wa Yanga aliyerithi majukumu hayo kutoka kwa Shadrack Nsajigwa.
  • Donald Ngoma, Thabani Kamusoko, Vicent Bosou, Isoufou Boubabakar, Paul Nonga, Geofrey Mwashiuya, Deus Kaseke, Haji Mwinyi, Benedict Tinoco na Matheo Anthony ni wachezaji ambao wametwaa taji hilo kwa mara ya kwanza baada ya kujiunga na Yanga msimu huu.
  • Yanga walitangaza ubingwa wakiwa na pointi 68 baada ya Simba kupoteza mchezo wao dhidi ya Mwadui, leo walikuwa wanakabidhiwa kombe hilo bila kujali kama wangefungwa, kutoka sare au kushinda dhidi ya Ndanda FC.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.