Ligi Kuu ya kandanda Tanzania Bara (VPL) itafikia mwisho wikendi ijayo kwa timu zote 16 kucheza game zao za 30.
Tayari bingwa wa msimu huu amekwisha fahamika (Yanga) ambao watakabidhiwa kombe lao siku ya Leo. Hapa nakuletea thamani ya zawadi mbalimbali ambazo wadhamini wakuu wa ligi hiyo kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom watazitoa kwa washindi.
BINGWA KULAMBA TSH. 81 MIL
Yanga itaingiza zaidi ya milioni 81 katika akaunti yao kutokana na kutwaa kwao taji hilo.
MSHINDI WA PILI
Mshindi wa pili katika ligi hiyo anataraji kuvuna kiasi cha milioni 40. Nafasi hii hadi sasa inawaniwa na timu za Azam FC na Simba.
MSHINDI WA TATU
Timu itakayomaliza nafasi ya tatu yenyewe itafanikiwa kujipatia kiasi cha milion 29.
MSHINDI WA NNE
Mtibwa Sugar ikiwa itamaliza katika nafasi ya nne waliyopo kabla ya game mbili za mwisho inaweza kupata milioni 23 kama zawadi ya mshindi wa nafasi hiyo.
MFUNGAJI BORA
Mrundi, Amis Tambwe anasaka tuzo yake ya pili ya ufungaji bora katika VPL. Akiwa amekwishafunga jumla ya magoli 21 hadi sasa, mfungaji huyo bora wa msimu wa 2013/14 anaweza kujiingizia kiasi cha milioni 5.4 kama zawadi ya mfungaji bora.
MCHEZAJI BORA WA LIGI
Mshindi wa tuzo hii msimu uliopita ni kiungo mshambulizi wa Yanga, Saimon Msuva. Unajua mchezaji bora wa msimu atavuna kiasi gani? Ni kiasi cha milioni 5.4.
GOLIKIPA BORA
Kama ilivyo kwa mfungaji bora na mchezaji bora wa msimu, tuzo ya kipa bora pia itaambatana na zawadi ya milioni 5.4.
TIMU YENYE NIDHAMU
Klabu yenye kadi chache na iliyoonyesha uungwana kwa msimu mzima itazawadiwa kiasi cha milion 17.
KOCHA BORA
Tuzo hii ilizua maneno mengi msimu uliopita baada ya Mbwana Makatta aliyekuwa ameisimamia Kagera Sugar kutangazwa mshindi licha ya kwamba alikuwa katika msimu kwa game nane tu. Tuzo ya kocha bora itaendana na zawadi ya milioni 8.
MWAMUZI BORA
Mwamuzi atakayekuwa amefanya vizuri kwa msimu mzima atazawadiwa tuzo na kiasi cha milioni 8 pesa taslim.

Maoni
Chapisha Maoni