Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JAJI LUBUVA ATAJA SABABU MBILI KUAHIRISHWA KURA YA MAONI KATIBA MPYA

JAJI LUBUVA ATAJA SABABU MBILI KUAHIRISHWA KURA YA MAONI KATIBA MPYA

Akizungumza leo Ikulu jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji mstaafu Damian Lubuva wakati akimkabidhi Rais Magufuli ripoti ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana alisema kuwa mchakato wa katiba mpya utaendelea.
Jaji Lubuva alizitaja sababu mbili za kuahirishwa kwa mkachakato wa kupiga kura ya maoni. Sababu hizo ni;-
  1. Kutokamilika kwa uandikishwaji wa wananchi kwa ajili ya kupiga kura. Jaji Lubuva alisema kuwa mchakato huo uliokuwa ufanyike Aprili mwaka 2015, uliahirishwa kwa sababu hadi siku ya kupiga kura ya maoni si wananchi wote waliokuwa tayari wameandikishwa. Hivyo kama mchakato huo ungeendelea ni dhahiri kuwa kuna wananchi ambao wangeshindwa kutimiza haki yao hiyo ya msingi.
2. Sababu ya pili ni uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Jaji Lubuva alisema kuwa Tume ya Taifa ya  Uchaguzi isingeweza kufanya vitu vyote viwili kwa wakati mmoja. Hivyo tume hiyo iliwasilisha serikali mapendekezo ya kuahirisha kura hiyo ya maoni hadi hapo uchaguzi utakapomalizika.
Akihitimisha hotuba yake, Jaji Lubuva alisema kuwa zoezi la upigaji wa kura za maoni sio kweli kwamba lilitelekezwa, bali liliahirishwa kwa sababu hizo mbili. Aidha alisema kuwa zoezi hilo lipo kwenye mchakato  na mara taratibu zote zitakapokamilika basi wananchi watapata fursa ya kupigia kura katiba mpya inayopendekezwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.