Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA CONTE AJIPA MATUMAINI ITALY KUWA MABINGWA


KOCHA wa Italy Antonio Conte anaamini Timu yake isiyopewa matumaini inaweza kuwaumiza Mabingwa Watetezi Spain ambao watacheza nao Jumatatu ijayo kwenye Mechi ya Raundi ya Mtoano ya EURO 2016 huko France.
Mechi hiyo itakuwa ni kama marudiano ya Fainali ya EURO 2012 iliyochezwa huko Kiev, Ukraine na Italy kubamizwa 4-0 na Spain waliotwaa Ubingwa.
Lakini Kocha Conte, ambae mara baada ya EURO 2016 anaondoka Italy na kutua London kuwa Meneja Mpya wa Klabu ya Chelsea, amesema Kikosi chake kiko imara hasa baada ya kuitwanga Timu ngumu ya Belgium 2-0 katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi lao la EURO 2016.
Italy walifuzu na kushika Nafasi ya Kwanza ya Kundi hilo baada ya Mechi 2 tu na kwenye Mechi yao ya mwisho Conte alibadili Wachezaji 8 na kufungwa 1-0 na Republic of Ireland.
Italy hawana rekodi nzuri dhidi ya Spain kwa Miaka ya hivi karibuni kwani pia walibwagwa kwa Penati kwenye Robo Fainali ya EURO 2008 ambayo pia Spain walibeba Kombe.
Na hata kama Italy wataibwaga Spain hiyo Jumatatu njia yao ya kutwaa EURO 2016 ni ngumu mno kwani Robo Fainali huenda wakakumbana na Mabingwa wa Dunia Germany na wakipita Nusu Fainali huenda wakawakwaa Wenyeji France au England.
EURO 2016
Ratiba
**Saa za Bongo
RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16
Jumamosi Juni 25
Switzerland v Poland (1600, Stade Geoffroy Guichard, St Etienne)
Wales v Northern Ireland (1900, Parc des Princes, Paris)
Croatia v Portugal (2200, Stade Bollaert-Delelis, Lens)
Jumapili Juni 26
France v Republic of Ireland (1600, Stade de Lyon)
Germany v Slovakia (1900, Stade Pierre Mauroy, Lille)
Hungary v Belgium (2200, Stadium de Toulouse)
Jumatatu Juni 27
Italy v Spain (1900, Stade de France, Paris)
England v Iceland (2200, Stade de Nice)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.