Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA Laurent Blanc ameachana na Paris Saint-Germain


KOCHA Laurent Blanc ameachana na Paris Saint-Germain baada ya kukubaliana Malipo ya EURO Milioni 22 (£17m) kama ‘Kiinua Mgongo’ kwa Mujibu wa Gazeti la Michezo la Ufaransa L'Equipe.
Blanc alionekana yuko mashakani huko PSG tangu Wiki 3 zilizopita pale Rais wa Klabu hiyo Nasser al Khelaifi alipoelezea kuwa Msimu wao wa 2015/16 ulifeli kwa sababu ya wao kutupwa nje ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Manchester City kwenye Hatua ya Robo Fainali.
Lakini, Nyumbani kwao France, PSG walifanikiwa kutwaa Trebo kwa mara ya Pili mfululizo walipobeba Ubingwa wa Ligi 1, Kombe la France na Kombe la Ligi.
Hata hivyo, kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI, PSG wamekuwa wakigota mwamba Hatua ya Robo Fainali kwa Misimu Minne mfululizo.
Blanc, Beki wa zamani wa France alietwaa Kombe la Dunia Mwaka 1998 na ambae pia aliwahi kuifundisha Timu ya Taifa ya France, alishika wadhifa PSG Mwaka 2013 baada ya Carlo Ancelotti kuondoka.
Blanc aliichezea Manchester United kwa Miaka Miwili na kufikisha Mechi 75 kati ya 2001 na 2003.
Blanc alisaini nyongeza ya Mkataba na PSG Mwezi Februari lakini, L'Equipe limesema ameondolewa PSG tangu Jana Jumatano huku ripoti zikiibuka kuwa Kocha wa Klabu ya La Liga huko Spain Sevilla, Unai Emery, ndie atashika wadhifa hapo PSG.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.