Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Marais wanne wanaosisitiza nidhamu kwa kiwango cha juu zaidi katika utumishi wa umma barani Afrika

Marais wanne wanaosisitiza nidhamu kwa kiwango cha juu zaidi katika utumishi wa umma barani Afrika

Kwa kawaida Marais wanatakiwa kutumia mamlaka yao kwa neema na pia uwezo wa  kujizuia iwezekanavyo lakini wakati mwingine , Kamanda mkuu anaweza akarudi na kuwa muongozaji mkuu wa nidhamu .  Hapa tumeweka orodha ya Marais wane wanaosisitiza nidhamu kwa kiwango cha juu zaidi katika utumishi wa umma barani Afrika.

Kufanyia kazi chini ya Marais hawa wa Afrika  hatuwezi kusema ni moja ya kazi rahisi duniani. Hawana simile kwa wafanyakazi wasiokuwa kwenye msitari na huhakikisha adhabu inatolewa ipasavyo kwa mhusika. Ni waadabishaji moja kwa moja kutoka moyoni na kwao, kitu cha muhimu zaidi kwao  ni kuhakikisha walicho kiagiza kimefuatwa ipasavyo na kimefanyika kwa ufanisi.
KagameRais  Paul Kagame wa Rwanda
Rais Paul Kagame hajafanya siri kuwa na kiu ya kuibadilisha Rwanda kuwa yenye mafanikio kwa kipindi alichokipanga na anaendelea vizuri mpaka sasa. Kiuchumi, Rwanda imeweka rekodi nzuri sana ya mapato ya Taifa (GDP) namba ya ukuaji wake na nafasi yake katika uchumi wa Dunia imekua ni ya kuonewa wivu na majirani zake wengi kutoka nchi za Afrika Mashariki.

Haya yote yamewezekana kutokana na uongozi wa Kagame na maadili ya kazi. Kwa kuongelea maadili ya kazi, Gazeti la New York Times liliwahi kuripoti kwamba, “hukaa mpaka saa nane au saa tisa za usiku kufuatilia mambo yalioko ‘The Economist’ au akisoma maendeleo ya ripoti za vijiji vya red-dirt vilivyoko katika nchi yake, huku akitafuta njia nzuri zaidi za kuweza kuongeza na kupanua Bilioni zinazopatikana katika Serikali yake kila mwaka kutoka kwa Nchi za wafadhili ambao humuweka kama mfano mzuri sana wa jinsi fedha za wafadhili zinavyoweza kufanya kazi nzuri Afrika.
David Himbara, mwandani wa zamani wa Kagame ambaye sasa anaishi uhamishoni nchini Afrika Kusini.

Himbara anasimulia jinsi Kagame ilivyo wahi kumuita mkurugenzi wa fedha na afisa wa jeshi katika ofisi yake mwaka 2009, na kumsema kuhusu ununuzi wa mapazia ya ofisi na baadae akaita walinzi wawili katika ofisi yake na fimbo na kuwaambia walale chini na kisha kuanza kuwachapa kwa hasira na alipochoka akawakabidhi viboko walinzi wake kuendelea kuwachapa.

Alipoulizwa kuhusu upigaji wake, Kagame hakukataa bali alisema “It’s my nature.” I can be very tough, I can make mistakes like that.”
President-Buhari-AURais Muhammadu Buhari wa Nigeria
Kama ilivyokua kwa Kagame, Rais Muhammadu Buhari nae yuko katika harakati za kuiweka nchi yake katika njia sahihi na hakika ya maendeleo kiuchumi. Kama Kagame pia yeye aliwahi kuwa mwanajeshi na alikuwa na sifa kubwa sana ya ukali na anapoagizwa alitekeleza kwa ufanisi na kuleta matokeo. Katika kipindi chake cha kwanza kama kiongozi wa Jeshi Nigeria mwaka 1984, Buhari alikuza sana sifa yake kuwa mwenye kunyoosha nidhamu sana.

Ilikuwa ni katika kipindi chake cha kwanza alipoanzisha kile alichokiita ‘vita dhidi ya utovu wa nidhamu’ katika jitihada za kutaka Wanigeria wapitishe misingi ya kiraia kama kupanda mistari kwenye vituo vya mabasi. Alifanisha hili baada ya kupeleka wanajeshi wenye viboko kwenye vituo hivyo vya mabasi.

Vile vile ‘Vita dhidi ya watovu wa nidhamu’ iligusa hadi wafanyakazi walio chini ya Buhari. Kwa kipindi hicho, watumishi wa Serikali waliofika kazini wamechelewa walirushwa kichura chura ikiwa kama adhabu ya uchelewaji wao.

Na sasa kuna fununu kwamba Buhari anataka kufufua ‘Vita dhidi ya Utovu wa nidhamu’ na kuianzisha upya. Waziri wa Habari na utamaduni Alhaji Lai Mohammed alisema kampeni hizo zitapewa jina ‘mabadiliko huanza na mimi’ na itakua hususani kwa ajili ya kuongeza uadilifu maadili ya kazi kwa ujumla Nidhamu katika Nchi.

Na kama itakua kama ilivyokua mwanzoni, kampeni hii mpya ya uongozi wa Buhari itatikisa sana watumishi wa Umma.
jpRais John Pombe Magufuli wa  Tanzania
John Pombe Magufuli  kwa sasa inawezekana akawa anaongoza kwa kukubalika kuliko Rais yeyote Afrika. Tangu ale Kiapo cha kuongoza Ofisi ya Rais mwaka jana Novemba, amekua katika vita ya kuindoa rushwa, Uzembe na Utoro katika nchi yake.

 Alifuta sherehe za uhuru na kuongoza usafi wa mitaa badala yake na vile vile akakata bajeti ya chakula cha usiku iliyopangwa kufanyika kwa ajili ya ufunguzi wa Bunge kwa 90%, na vile vile kutaja idadi pungufu ya mawaziri 11 ya Baraza la mawaziri lilokuwepo kabla ya uongozi wake.

Watanzania wamempenda na kufurahia uongozi wa Magufuli kiasi cha kumpa jina la Tinga Tinga, kwa kile ambacho wanasema hana upendeleo wowote aliteka pia mitandao ya kijamii katika Afrika mashariki mfano Twitter kulianzishwa Hashtag ya  #WhatWouldMagufuliDo, msemo ulitokana na jinsi alivyokua akipunguza matumizi kwa vitu visivyo na umuhimu.

Kwake yeye fuata taratibu, na ameshatuonyesha ni jinsi gani usipofuata taratibu ni nini kinatokea. Tangu kuapishwa kwake, Magufuli amesha fukuza watu zaidi 150 katika nyazifa mbalimbaliza kazi, ikiwa ni pamoja na kiongozi mkuu wa kuzuia na kupambana na rushwa. Na wala hajaacha wale aliokua nao karibu kwa lolote. Hivi karibuni alimfukuza Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga, ambaye ni Rafiki yake wa karibu kwa kuingia Bungeni  amelewa.

South Sudan's President Salva Kiir attends a one-day summit on oil on September 3, 2013 in Khartoum. Sudan and South Sudan averted a shutdown of economically vital oil flows and again pledged to implement economic and security pacts that have twice failed to take effect.  AFP PHOTO / ASHRAF SHAZLY        (Photo credit should read ASHRAF SHAZLY/AFP/Getty Images)
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini
Rais huyu wa Sudan Kusini ameingia katika ukurasa wetu huu kwa hisani ya post zilizowekwa Facebook na Mabior Garang de Mabior, mtoto wa aliyekuwa mwanzilishi wa Nchi ya Sudan Kusini

Dr. John Garang de Mabior. Kijana huyo Garang, ambae ni Waziri wa vyanzo vya maji alipost Facebook jinsi alivyofukuzwa katika mkutano wa baraza la mawaziri na Rais akiwa amevaa Bow tie.
Kiir ameweka mavazi ya kuvaa kwa mawaziri wake, na bow tai si moja wapo. Lazima iwe tai ya kawaida.

Na hao ndio Viongozi wane Afrika, wanaongoza kwa kuzingatia Nidhamu. Inaweza kuwa jinsi ya kutenda na Usimamizi wake ukawa sio wa kawaida, lakini vichwani mwao wakawa wanaona ni sahihi kwa zile changamoto Nchi zao zinakabiliana nazo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.