Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wayne Rooney amemtetea Roy Hodgson


KEPTENI wa England Wayne Rooney amemtetea Meneja wake Roy Hodgson na kusisitiza Wachezaji wote wanaheshimu uamuzi wake wa kubadili Wachezaji 6 walipotoka Sare 0-0 na Slovakia Juzi Jumatatu katika Mechi ya Kundi B la EURO 2016 huko France.
Licha ya kuwepo ripoti kuwa Rooney, ambae aliingizwa Kipindi cha Pili kwenye Mechi hiyo na Slovakia, alishangazwa na kutemwa kwake, mwenyewe Rooney amesisitiza Kambi ya England iko burdani.
Rooney ameeleza: “Naheshimu uamuzi wa Roy. Kama Mchezaji unataka kucheza lakini kwenye Raundi ijayo dhidi ya Iceland nitakuwa freshi zaidi!”
Mbali ya kupumzishwa Rooney kwenye Mechi hiyo na Slovakia, Hodgson pia aliwatema Kyle Walker, Danny Rose, Dele Alli, Raheem Sterling na Harry Kane na Droo hiyo ikatoa mwanya kwa Wales kutwaa ushindi wa Kundi B.
Hilo likafanya Wales waikwae Northern Ireland kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya EURO 2016 na England wataivaa Iceland kwenye Raundi hiyo hiyo Jumatatu ijayo huku Washindi wakitinga Robo Fainali.
Rooney ameongeza: “Nadhani ni uamuzi ambao Roy alifanya ili kupumzisha Wachezaji na kwa kuamini Kikosi chake. Nakubaliana nao. Wachezaji waliopangwa hawakuwa wazuri kushinda Mechi lakini vile vile wapinzani walijihami vizuri.”
Ikiwa Rooney atacheza Jumatatu ijayo dhidi ya Iceland, itakuwa Gemu yake ya 115 kwa England akifungana na David Beckham na kuwa wa Pili katika Listi ya Kihistoria ya Wachezaji waliochezea Mechi nyingi England ambayo inaongozwa na Kipa Peter Shilton aliecheza Mechi 125.
Rooney ameeleza: “Nimesema mara nyingi kwamba ni heshima kubwa kuwa Kepteni wa Nchi yangu na ni kitu daima najaribu kukifanya kwa uwezo wangu wote na kwa fahari kubwa!”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.