Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Amsubiri mpenziwe siku 10 katika uwanja wa ndege

Amsubiri mpenziwe siku 10 katika uwanja wa ndege

Image captionAsubiri mpenziwe siku 10 katika uwanja wa ndege
Je penzi la kweli lipo ?
Hilo ndilo swali linaloulizwa sana katika mitandao nchini China.
Hii ni baada ya raia mmoja kutoka Uholanzi kusafiri maelfu ya kilomita ili kukutana na mpenziwe raia wa uchina ambaye walikutana kwenye mitandao ya kijamii.
Hata hivyo mpenziwe hakujitokeza hata baada ya kusubiri katika uwanja wa ndege kwa siku 10!
Amini usiamini alimsubiri kwa siku 10!
Alexander Pieter Cirk, 41, alifunga safari hadi jimbo la Hunan kukutana na mpenziwe mwanamke kutoka Uchina ambaye anafahamika kwa jina Zhang.
Image captionbi Zhang mwenye umri wa miaka 26 anasema alidhania kuwa ulikuwa ni mzaha tu
Na baada ya kumsubiri kwa siku kumi katika uwanja wa ndege wa Changsha hakujitokeza ,,Cirk alienda kufanya subira na mwishowe akalazimika kulazwa hospitalini kwa uchovu wa mwili na roho.
Cirk ameviambia vyombo vya habari kuwa walikutana na bi Zhang mwenye umri wa miaka 26 miezi miwili iliyopita na penzi lao likachipuka.
Hata hivyo alipofika China akagundua kuwa wanawake wengi nchini humo wanafanana, na akashindwa kumpata Zhang kwa simu.
Ripoti hiyo ilipopeperushwa kwenye runinga ya taifa , bi Zhang alijitokeza na kuwaamnbia Wachina kuwa alidhania kuwa ni utani tu kama vile maisha ya mjini kwa wanawake wengi ambao huambiwa kuwa wanapendwa.
''Ni kweli kuwa tulikuwa tunapendana lakini nilianza kumshuku huenda alikuwa ananichezea shere''
Alinitumia picha za tiketi ya ndege na hakunipigia simu baada ya hapo''
Kwa hivyo nikapuuza nikijua kuwa ni mzaha tu''bi Zhang aliiambia Hunan TV.
Image captionAlexander Pieter Cirk alilazwa hospitalini baada ya kuzimia
Zhang alisema kuwa ule wakati alipokuwa akimtarajia ,yeye alikuwa amefanyiwa upasuaji katika mji mwengine wa mbali.
Hangeweza kumpokea katika uwanja wa ndege.
katika mitandao ya kijamii tukio hilo limewaacha wengi wasijue iwapo ilikuwa ni penzi la kweli ama ni ujinga wa kuzaliwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.