Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kampeni zaanza kupamba moto Marekani

Kampeni zaanza kupamba moto Marekani

Image copyrightGIBORN
Watu wenye ushawishi pamwe na wanasiasa maarufu nchini Marekani kutoka katika bunge la Congress na chama cha Republican wametoa matamko yao kuwa hawatampa kura zao mgombea wa nafasi ya urais Donald Trump, wakisema kwamba mgombea huyo hatoshi kwa nafasi hiyo nyeti ulimwenguni.
Mapema wiki hii, Richard Hanna kutoka mjini New York amekuwa mwanachama wa kwanza kutoka chama cha Republican kutamka hadharani kuwa atampa kura yake mgombea wa kiti cha urais kutoka chama cha Democrat Hillary Clinton.
Hanna amemwita Donald Trump aibu ya taifa, wanachama wengine kutoka chama cha Republican wamejitenga kutomshabikia Trump ama hata kutomuunga mkono.
Kauli za Donald Trump,sera zake dhidi ya wanawake,masuala ya wahamiaji wasiokuwa na nyaraka zinazotakiwa na Waislamu hayawaingii kichwani viongozi walio wengi kutoka upande wa chama cha Republican.
Image copyrightGIBORN
Katika hatua nyingine rais Barack Obama amemshambulia mgombea huyo wa nafasi ya urais kwa tiketi ya chama cha Republican, Donald Trump, kwa madai ya kutokuwa na sifa stahiki kuwa rais wa Marekani.
Obama hakuishia hapo bali amewashangaa wafuasi wa chama cha Republican kwanini wanendelea kumuunga mkono mgombea huyo, amesema kwamba Trump amekuwa ni tofauti na wagombea waliopita wa chama cha Republican kama alivyo Mr Trump namna anavyotoa hukumu ama tabia zake za kuajabisha ambazo haziendani na mtu anayetarajiwa kuchukua madaraka makuwa na yenye nguvu kubwa zaidi katika dunia.
Naye Donald Trump hakuacha maneno hayo yapite bure bali alijibu mashambulizi kwa kumshutumu raisi Barack Obama kama kiongozi aliyeshindwa na kwamba mgombea anayetaka kurithi nafasi yake Hillary Clinton, naye hafai kuwania nafasi hiyo ama hata katika ofisi yoyote ile ya serikali.
WAKATI HUO HUO
Wakati vita vya maneno katika kampeni hizo vikipamba moto, mkuu wa kamati kuu ya chama cha Democratic nchini Marekani amejiuzulu nafasi hiyo. Uamuzi huo wa Amy Dacey kujiuzulu unafutia kuvuja kwa maelfu ya barua pepe zenye kuonesha mapendekezo ya chama cha Democratic dhidhi ya njama za makusudi za kudhoofisha kampeni ya Hillary Clinton dhidi ya mpinzani wake wa zamani Bernie Sanders aliyekuwa mgombea urais.
Dacey kuachia ngazi kwake anakuwa mtu wa pili kujiuzulu baada ya mwenyekiti wa wanawake wa chama hicho , Debbie Wasserman Schultz,kabla ya mkutano mkuu wa taifa wa chama cha Demokratic mjini Philadelphia wiki iliyopita.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.