Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAN CITY yashinda tano UEFA


Aguero akipunga mkono baada ya kutupia wavuni.
Manchester City imeanza vizuri kampeni zake za kuwania kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kutoa kipigo kikali kwa Steaua Bucharest cha mabao 5-0 licha ya kuwa matajiri hao wa Jiji la Manchester walikuwa ugenini.
Kipa wa Man City, Caballero akipongezana na kiungo wake Fernandinho mara baada ya mchezo huo.


Katika mchezo huo ambao ulitawaliwa na Man City kwa asilimia kubwa Kocha Pep Guardiola alionekana kuw ana kazi nyepesi ya kuwapa maelekezo wachezaji wake kwa kuwa upinzani ulikuwa ni wa kiwango cha chini kiasi kwamba City ni kama walikuwa mazoezini. 

Ndani ya kipute hicho ambacho ilishuhudiwa kipa namba moja wa Man City, Joe Hart akiendelea kusugua benchi, straika Sergio Kun Aguero alifunga mabao matatu huku akikosa penalti pia.

Aguero alifunga mabao hati katika dakika ya 41, 78 na 89, wakati ambapo mabao mengine yaliwekwa wavuni na David Silva dakika ya 12 na Nolito dakika ya 49.

Timu hizo zitarudiana Agosti 24, mwaka huu na baada ya hapo itafuata hatua ya makundi rasmi.

Matokeo mengine ya mechi hizo za kuania kufuzu hatua ya makundi yalikuwa hivi:

Ajax 1 – 1 FC Rostov
Dinamo Zagreb 1 – 1 Salzburg
FC Koebenhavn 1 – 0 APOEL Nicosia
Young Boys 1 – 3 Borussia Moenchengladbach


Guardiola akitoa maelekezo.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.