Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mario Götze arudi Borussia Dortmund

Borussia Dortmund Bayern München 2013 am 5. Mai 2013

Mshambuliaji wa Ujerumani Mario Götze kawaida ataonekana na baadhi ya mashabiki wa Borussia Dortmund kuwa ni “Yuda”, ambao hawajafurahishwa na habari kuwa amerejea
Wengine hata hivyo wanaamini kuwa anaweza kuwa mtu wa kujaza pengo lililoachwa na Henrikh Mkhitaryan.
Baadhi ya wachambuzi wa kandanda la Bundesliga na mashabiki wa Dortmund wanaonekana kukubaliana na msemo wa jadi kuwa “Usiwahi kurudi nyuma”:
Uamuzi wa Götze kuhama Dortmund na kujiunga na mahasimu wao wakuu Bayern Munich mwaka wa 2013 haukuchukuliwa vyema katika uwana wa Signal Iduna Park, na sasa ana kibarua cha kurejea na kujega upya mahusiano yaliyovunjika.
Lakini mashabiki wengine wengi wa BVB wakiongozwa na kocha Thomas Tuchel wameelezea matumini kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 atakuwa na mchango mkubwa "Tunatumai ataleta kipaji chake. Ningependa kumwona Mario akicheka kila wakati na tena tufahamiane vyema. Nna uhakika kuwa mara tu atapoanza kucheza, ataweza kuimarika na kuwa atadhihirisha yeye ni mchezaji wa kuvutia".
Götze alishinda mataji mawili ya Bundesliga akiwa na Dortmund kabla ya kujiunga na Bayern, lakini akashindwa kupata nafasi katika kikosi cha kwanza chini ya kocha Pep Guardiola aliyehamia Manchester City ya England.
Mario Götze Fußball zurück zum BVB
Baadhi ya mashabiki hawakufurahia uhamisho wa Götze
Mats Hummels pia aliondoka Dortmund akiwa mchezaji wa tatu nyota kujiunga na Bayern baada ya Götze na Robert Lewandowski. Lakini baada ya Götze kurejea Dortmund na Sebastian Rode pia kuhama Bayern na kujiunga na Dortmund, mambo yameonekana kubadilika. Itabakia kuona kama hiyo itakuwa na mchango wowote kwenye kinyang'anyiro cha taji la Bundesliga au la.
Na siku moja tu baada ya tangazo la Götze kurejea BVB, klabu hiyo imetangaza kumsaini winga wa Ujerumani Andre Schürrle kutoka mahasimu wao wa Bundesliga, Wolfsburg. Schürrle mwenye umri wa miaka 25 amesaini mkataba wa miaka mitano hadi mwaka wa 2021 na ataanza kufanya mazoezi na klabu hiyo mwezi Agosti.
Alianzia mpira wake Mainz, mwaka wa 2009 kabla ya kujiunga na Bayer Leverkusen 2011 kwa miaka miwili. Alijiunga na Chelsea ya England mwaka wa 2013 kabla ya kusainiwa na Wolfsburg Januari 2015.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.