Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Serikali ya Tanzania kukata rufaa ndoa za utotoni

Serikali ya Tanzania kukata rufaa ndoa za utotoni


Serikali ya Tanzania imewasilisha ombi la kukata rufaa, uamuzi wa kihistoria nchini uliopinga ndoa za watoto walio chini ya umri wa miaka 18.Mwezi uliopita mahakama kuu iliamua kuwa sehemu za sheria ya ndoa mwaka 1971, iliyoruhusu wasichana kuolewa wakiwa na umri wa hata miaka 14 ni kinyume na katiba.
Kundi la kutetea haki za watoto "Msichana Initiative" iliwasilisha kesi hiyo mahakamani. Taarifa hiyo ya kukata rufaa imewashtusha wengi Tanzania , wengi wakishindwa kuelewa ni kwanini mkuu wa sheria angetaka kugeuza hukumu hiyo.
Mwezi uliopita mahakama kuu iliipa serikali muda wa mwaka mmoja kurekebisha kosa hilo na kuweka umri wa miaka 18 kama umri sahihi wa watu kufunga ndoa, kwa wote wasichana na wavulana nchini.
Awali sheria ya ndoa ya mwaka 1971 nchini Tanzania imetaja kuwa wavulana wanapaswa kuoa wakiwana miaka 18 huku wasichana wakiwa na umri wa miaka 15. Kesi hiyo iliwasilishwa na kundi la kutetea haki za watoto Msichana Initiative, kupitia wakili Jebra Kambole.
Asilimia 37 ya wasichana walio na umri wa chini huolewa Tanzania. Wasichana wenye umri wa hata miaka 14 huozwa kwa idhini ya wazazi. Na wengi wao baadaye huripotiwa kukabiliwa na unyanyasaji nyumbani na hutengwa katika jamii - wakikosa nafasi za kusoma na kuajiriwa.
Hivi karibuni bunge lilikarabati kipengee cha sheria ya elimu na sasa ina sehemu inayotoa hukumu ya kifungo cha miaka 30 gerezani au faini ya dola 2500 kwa wanaume wanaowapachika mimba au kuwaoa wasichana wa shule.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.