Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Usain Bolt aandikisha historia katika Olimpiki

Mwanariadaha wa Jamaica Usain Bolt ndiye mshindi wa mbio za mita 100 katika mashindano ya Olimpiki ya Rio baada ya kuzimaliza mbio hizo kwa sekunde 9.81 dhidi ya mshindani wake wa karibu, Justin Gatlin.
Bolt ameingia katika kumbukumbu za historia kwa kuwa mwanariadha pekee katika historia ya miaka 120 ya olimpiki, kushinda medali ya dhahabu mara tatu mfululizo katika mashindano ya mbio za mita 100.
Bolt alishinda mara ya kwanza medali ya dhahabu mwaka 2008 mjini Beijing na kisha London mwaka 2012. Mwanariadha huyo wa Jamaica mwenye umri wa miaka 29 amesema anatazamia ushindi mwingine katika mashindano ya mbio za mita 200 na za mita 100 kupokezana vijiti wiki hii ili kumfanya mtu asiyeshaulika.
Nani kama Bolt?
Punde baada ya kushinda, Bolt amewaambia wanahabari kuwa hii ndiyo sababu alishiriki, kuuthibitishia ulimwengu kuwa ndiye mwanariadha bora zaidi na kuongeza amefurahi na anajivunia ushindi wake. Mwanariadha huyo anayeshikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 100 amesema atastaafu baada ya michuano ya ubingwa dunia mwaka 2017.
Usain Bolt na mshindani wake wa karibu Justin Gatlin
Usain Bolt na mshindani wake wa karibu Justin Gatlin
Maelfu ya watu walimiminika mitaani nchini Jamaica licha ya barabara kujaa tope baada ya mvua kubwa kusherehekea ushindi wa Bolt.
Lakini si Usain Bolt pekee ambaye amevunja rekodi usiku wa kuamkia leo katika mashindano ya olimpiki ya Rio. Mwanariadha wa Afrika Kusini Wayde van Niekerk ameandikia rekodi ya kuzikamilisha mbio za mita 400 kwa muda wa sekunde 43.03 na kujinyakulia medali ya dhahabu.
Van Niekerk amevunja rekodi iliyowekwa na Johnson ya sekunde 43.18 mwaka 1999. Van Niekerk mwenye umri wa miaka 24 aliwaduwaza washindani wake wa karibu Krinadi James wa Grenada aliyemaliza mashidano hayo kwa muda wa sekunde 43.76 na mshindi wa medali ya dhahabu wa mashindano ya olimpiki ya 2008 La Shawn Meritt wa Marekani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.