Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga Vs Azam Ngao ya Jamii 2016

Bonge la mechi ya kisasi leo linatarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa kuwakutanisha mabingwa watetezi Yanga watakaovaana na wapinzani wao, Azam FC kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii.

Mechi hiyo hatachomoka mtu kwa kuwa ni lazima timu moja ipate ushindi aidha kwa dakika tisini au kwenye mikwaju ya penalti.


Katika mechi hiyo Azam wataingia uwanjani kwa kazi moja pekee ya kulipa kisasi baada ya mara mbili zote walizokutana katika Ngao ya Jamii kufungwa.

Wataingia uwanjani wakiwa na benchi jipya la ufundi linaloongozwa na Mhispania, Zeben Hernandez aliyetua nchini hivi karibuni akirithi mikoba ya Muingereza, Stewart Hall aliyesitishiwa mkataba wa kuendelea kukinoa kikosi hicho.

Akizungumza na Championi Jumatano kocha wa Yanga, Hans van Pluijm alisema kikubwa yeye anataka kuendeleza rekodi yake ya kuchukua mataji kwa kuanza hili la Ngao ya Jamii.

Pluijm alisema, taji hilo la Ngao la Jamii anataka kulichukua ili atengeneze mwanzo mzuri katika kulitetea taji lao la ubingwa wa ligi kuu na Kombe la FA, hiyo ni kutokana na mabadiliko makubwa ya wachezaji waliyoyaonyesha hivi karibuni baada ya kupata uzoefu mkubwa.

"Ninataka kuanza na mwanzo mzuri kwa kuchukua Ngao ya Jamii dhidi ya Azam, licha ya kukabiliwa na changamoto moja ya wachezaji wangu kutumika kwa kipindi kirefu bila ya kupumzika tofauti na timu nyingine ambazo zimepata muda wa kupumzika.



  
"Kama unavyojua tupo kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, hivyo tulikosa muda kabisa wa kupumzika, lakini hiyo hainipi hofu kutokana na maandalizi niliyoyafanya ya kikosi changu, tutatumia uzoefu tulioupata kwenye michuano hiyo kuwafunga Azam.

"Ninafurahi mabadiliko makubwa ya kikosi changu kwa kuanzia safu ya ulinzi iliyokuwa ikikosa umakini katika kuokoa mipira ya krosi na kona na kusababisha kuruhusu mabao, lakini nafurahia mabadiliko makubwa hivi sasa," alisema Pluijm.

Hata hivyo, Yanga watakuwa na pigo kubwa leo kwa kuwa itawakosa mastaa wake watano ambao wanasumbuliwa na majeraha ambao ni Kelvin Yondan (jicho), Obrey Chirwa (goti), Juma Abdul (misuli), Ally Mustapha (kidole) na Vincent Andrew (nyonga).

  



  Kwa upande wa kocha wa Azam, Hernandez yeye ameweka wazi kuwa ana uhakika mkubwa wa kuifunga Yanga kwenye mchezo huo kutokana na maandalizi mazuri aliyoyafanya.

"Nisingependa kuzungumzia sana mechi ya Yanga kwani ninaamini kuwa, jitihada zangu na mafunzo yangu ninayowapa wachezaji wangu itazaa matunda, lakini natambua ya kuwa Yanga ni timu kongwe na inacheza vizuri.

"Kikubwa ninaamini nitashinda kwenye mchezo huu kutokana na kile ninachowapa wachezaji wangu na kikubwa, nimeweka mkazo kwenye baadhi ya sehemu kwa kuwapa mbinu mbadala zitakazotupa ushindi," alisema Hernandez.

CHANZO: CHAMPIONI

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.