Ruka hadi kwenye maudhui makuu

‘Nilikuwa natafuta goli la Europa League kuliko kitu chochote’ -Samatta


Baada ya Mbwana Samatta kuifungia magoli mawili timu yake ya Genk kwenye mashindano ya Europa League na kuisidia kupata ushindi wa magoli 5-2 ugenini dhidi ya Gent, Samatta amesema alikuwa anatafuta kufunga goli kwenye michuano hiyo kuliko kitu chochote kwa hiyo magoli hayo mawili yamekuja katika wakati muafaka.
“Nakosa kitu cha kusema ni jinsi gani nilivyojisikia kwa sababu nilikuwa natafuta hilo goli la Europa kuliko kitu chochote nilikuwa nahangaika, na kipindi nalitafuta hayo magoli yalikuwa hayaji, kwa hiyo hadi inafika ile game nilikuwa nimeshahangaika sana kutafuta magoli na magoli yenyewesipati. Nilikuwa natumia kila njia hadi nikaamua ku-relax na kuondoa hicho kitu ili mwili wangu utulie nifanye kazi kama inavyotakiwa,” anasema Samatta wakati akihojiwa na kipindi cha Sports Extra cha Clouds FM.
“Ilifika kipindi nikasema kama goli likija basi Mungu atakuwa ameleta baraka zake na lisipokuja basi kwa sababu nilikuwa naona kila napojaribu kulazimisha ndio nazidi kuumia na kwa sababu nachokitaka hakiji, nikaamua kumuachia Mungu, mimi nifanye kazi, kweli Mungu akaleta neema kwenye ile game. Nnadhani kikosi kilikuwa kizuri na mimi nilikua vizuri pia na nafasi zilikuwa zinapatikana.”
Magoli mawili aliyofunga Samatta kwenye mechi ya Europa League dhidi ya Gent yanamfanya kufikisha magoli manne kwenye michuano hiyo huku akiwa tayari amefikisha magoli 16 katika mashindano yote

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.