Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ushindi usio wa kishindo kwa Merkel


Angela Merkel anaonekana amechoka, alipowasili katika makao makuu ya chama chake baada ya kumalizika uchaguzi.
Akitoka katika gari lake alitabasamu kwanza kwa wapiga picha waliomsubiri alafu kwa wafuasi wa chama chake waliokusanyika katika makao ya chama cha CDU.
Kansela alitambua kwamba huenda angeshinda uchaguzi huu. Lakini sio ushindi alioutarajia yeye binfasi wala chama chake. Ni matokeo mabaya kwa chama hicho cha kihafidhina chini ya utawala wake.
Huenda ni matokeo ya uamuzi wake kuwafungulia mlango mamilioni ya wakimbizi kuingia Ujerumani.
Akihotubia wafuasi wa chama chake, Bi Merkel amekiri kwamba miaka minne iliyopita imekuwa migumu. Licha ya hayo chama chake kimefanikiwa kwa lengo lake - Kuibuka mshindi.
Nderemo hazikuwa kubwa kwasababau ushindi mkuu wa uchaguzi huu ni wa AfD.
Upande wa pili wa mji huo, katika chumba kilicho sheheni vibofu vya rangi ya samawati na nyeupe, wafuasi wa chama kinachopinga uhamiaji, kinachopinga Umoja wa Ulaya walisherehekea ilipobainika
kwamba hawatoingia bunge kwa mara ya kwanza tu, lakini kwamba watakuwa wafuasi wa chama cha tatu kwa ukubwa bungeni baada ya chama cha Merkel CDU na wapinzani wake wa karibu Social democratic - SPD.
Lakini kampeni ya ubaguzi ya AfD na ghasia zilizo tatiza mikutano ya Merkel huenda ni mfano wa yanatorajiwa. Nje ya makao ya chama hicho, maafisa wa polisi wana watazama kwa makini waandamanaji
wanaokipinga AfD dhidi ya kile wengi wanaona ni maendeleo ya kushtusha ya kisiasa.
Kuna migawanyiko, na hisia ya kutoridhia katika taifa hili. Baadhi wanatishiwa na wanachokitaja kuwa ni kukuwa kwa siasa za utaifa za mrengo wa kulia.
Bi Merkel sasa ni lazima atafuta washirika wa kuunda serikali ya muungano. Na ni lazima aishawishi nchi yake na pengine baadhi ndani ya chama chake, kwamba anastahili kazi hiyo.
Zimekuwa ni kampeni ndefu na za kutia uchungu. Huenda Merkel ameshinda lakini ushindi wake hauna kishindo
Uchaguzi huu utaingia katika vitabu vya historia kwa sababu mbili. Huenda Angela Merkel ameshinda hatamu ya nne uongozini lakini ni matokeo mabaya kuwahi kushuhudiwa kwa chama chake.
Na pili wanasiasa wa mrengo wa kulia wanaoshinikiza utaifa, sasa wamejiunga katika utawala wa Ujerumani.
Kilicho kawaida ya siasa katika nchi nyingine nyingi Ulaya kilichodhaniwa hakiwezi kufanyika katika Ujerumani ya baada ya vita vikuu. Sasa kimekuwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House

Trump: Tajiri anayetaka kuingia White House Image copyright GETTY Image caption Trump huamini sana katika kushinda Donald Trump ni tajiri anayemiliki majumba mengi na ambaye amekuwa mtangazaji wa kipindi cha maisha ya uhalisia kwenye runinga. Amekuwa mtu anayeangazia sana ushindi katika maisha yake na anasema ni lazima afanikiwe katika kupata tuzo kuu duniani, kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani. Tayari ameidhinishwa na chama cha Republican kuwania urais baada ya kuwabwaga wapinzani wengine. Kwa wafuasi wake, mgombea huyu wa Urais kwa chama cha Republican ndiye anayeweza kuleta ufanisi kwa Marekani. US: Maneno ya Trump ni hatari kwa usalama Kwao, huyu ni tajiri shupavu anayeweza kusuluhisha matatizo yote ya nchi ambayo wanahisi yameshusha hadhi ya Marekani duniani. Wengi wao ni raia wa Marekani wafanyikazi hasa wenye asili ya Kizungu na walio na maisha ya kadri. Mbaguzi na mfitini Hata hivyo kwa wakosoaji wake, wanasema huyu ni mbaguzi na mfitini, muonevu mkubwa amb...

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao

Haya ndo makundi ya Wachaga na tabia zao Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja.  Wachaga hutokea maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro na hua na tabia tofauti. Haya ni baadhi ya makundi ya wachaga na tabia zao. 1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”.. Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji. 2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu. 3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchi...

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Baada ya duru la tatu la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika kwa timu 16 kushuka katika viwanja mbali mbali kuzisaka pointi tatu muhimu mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 2000 klabu ya Mtibwa Sugar inashika msukani katika msimamo kwakuwa na alama 10. Kikosi cha timu ya Mtibwa Sugar Katika msimamo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendelea kufanya vizuri nakushika nafasi ya pili baada ya hapo jana Usiku kuifunga Lipuli FC. Klabu ya Singida United ambayo imepanda msimu huu ikiwa chini ya Mwalimu Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm inashika nafasi ya tatu na kuwazidi wakongwe klabu za Simba SC inayoshika nafasi ya nne na Young Africans inashika nafasi ya sita. Chati nzima ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.